+ -

عن عائشةَ أُمِّ المُؤْمِنينَ رضي الله عنها:
أن النبي صلى الله عليه وسلم كان لا يَدع أربعا قَبل الظهر وركعتين قبل الغَدَاة.

[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 1182]
المزيــد ...

Imenukuliwa kutoka kwa Aisha mama wa waumini radhi za Allah ziwe juu yake:
Yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake alikuwa haziachi rakaa nne kabla ya Adhuhuri na rakaa mbili kabla ya Alfajiri.

[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [صحيح البخاري - 1182]

Ufafanuzi

Ameeleza Aisha radhi za Allah ziwe juu yake yakuwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake alikuwa akidumu na swala za sunna ndani ya nyumba yake na wala haziachi: Rakaa nne kwa salamu mbili kabla ya swala ya Adhuhuri, na rakaa mbili kabla ya swala ya Alfajiri.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kireno Kiassam الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Sunna ya kuzihifadhi na kudumu na rakaa nne kabla ya swala ya Adhuhuri, na rakaa mbili kabla ya swala ya Alfajiri.
  2. Kilicho bora ni swala za sunna ziswaliwe nyumbani, na ndivyo alivyoeleza Aisha radhi za Allah ziwe juu yake.