عن عمران بن حصين رضي الله عنه قال: كَانَتْ بِي بَوَاسِيرُ، فَسَأَلْتُ النَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ عَنِ الصَّلَاةِ، فَقَالَ:
«صَلِّ قَائِمًا، فَإِنْ لَمْ تَسْتَطِعْ فَقَاعِدًا، فَإِنْ لَمْ تَسْتَطِعْ فَعَلَى جَنْبٍ».

[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 1117]
المزيــد ...

Kutoka kwa Imran bin Huswain -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Niliugua bawasiri, nikamuuliza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuhusu kusali, akasema:
"Swali ukiwa umesimama, usipoweza basi swali ukiwa umekaa, usipoweza basi ukiwa umelala ubavu".

[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [Swahiih Al Bukhaariy - 1117]

Ufafanuzi

Amebainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa asili katika swala ni kusali kwa kusimama, isipokuwa katika hali ya kutoweza hapo mtu atasali kwa kukaa, na ikiwa hatoweza kukaa atasali kwa ubavu.

Katika Faida za Hadithi

  1. Swala haidondoki kwa muda ambao akili bado ipo, itakuwa kwa kuhama kutoka hali moja kwenda nyingine kadiri ya uwezo.
  2. Huruma na wepesi wa Uislamu kwa kumpa uhuru mja afanye kadiri awezavyo katika ibada.
Kuonyesha Tarjama
Lugha: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Ziada (62)
Ziada