عن عمران بن حصين رضي الله عنه قال: كَانَتْ بِي بَوَاسِيرُ، فَسَأَلْتُ النَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ عَنِ الصَّلَاةِ، فَقَالَ:
«صَلِّ قَائِمًا، فَإِنْ لَمْ تَسْتَطِعْ فَقَاعِدًا، فَإِنْ لَمْ تَسْتَطِعْ فَعَلَى جَنْبٍ».  
                        
[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 1117]
                        
 المزيــد ... 
                    
Kutoka kwa Imran bin Huswain -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Niliugua bawasiri, nikamuuliza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuhusu kusali, akasema:
"Swali ukiwa umesimama, usipoweza basi swali ukiwa umekaa, usipoweza basi ukiwa umelala ubavu". 
                                                     
                                                                                                    
[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [صحيح البخاري - 1117]                                            
Amebainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa asili katika swala ni kusali kwa kusimama, isipokuwa katika hali ya kutoweza hapo mtu atasali kwa kukaa, na ikiwa hatoweza kukaa atasali kwa ubavu.