+ -

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ:
أَوْصَانِي خَلِيلِي صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ بِثَلاَثٍ: صِيَامِ ثَلاَثَةِ أَيَّامٍ مِنْ كُلِّ شَهْرٍ، وَرَكْعَتَيِ الضُّحَى، وَأَنْ أُوتِرَ قَبْلَ أَنْ أَنَامَ.

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 1981]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema:
"Aliniusia mimi kipenzi changu -rehema na amani ziwe juu yake kwa mambo matatu: kufunga siku tatu katika kila mwezi, na rakaa mbili baada ya kuchomoza jua (Dhuhaa), na nisali witiri kabla sijalala".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

Ufafanuzi

Anaeleza Abuu Huraira radhi za Allah ziwe juu yake yakuwa kipenzi chake na jamaa yake Mtume rehema na amani ziwe juu yake alimuusia na akamsisitizia mambo matatu:
La kwanza: Kufunga siku tatu katika kila mwezi.
La pili: Rakaa mbili za Dhuhaa kila siku.
La tatu: Kusali witiri kabla ya kulala; na hii ni kwa mtu atakayehofia kutoamka mwisho wa usiku.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Pashto Kiassam الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kutofautiana kwa usia wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake kwa Masahaba zake: Hii inasababishwa na elimu yake rehema na amani ziwe juu yake ya kujua hali za Masahaba zake, na kile kinachomfaa kila mmoja miongoni mwao, mwenye nguvu kinachomfaa ni Jihadi, na mchamungu kinachomfaa ni ibada, na mwanachuoni kinachomfaa ni elimu, na kuendelea.
  2. Amesema bin Hajari Al-Asqalaani: Katika kauli yake: Kufunga siku tatu katika kila mwezi, kinachoonekana nikuwa makusudio yake ni masiku meupe, ambayo ni: Siku ya tarehe kumi na tatu, kumi na nne, na kumi na tano, katika kalenda ya Hijiria.
  3. Amesema bin Hajari Al-Asqalani: Hapa inaonyesha kuwa inapendeza kuitanguliza witiri kabla ya kulala, na hii kwa mtu ambaye hana uhakika wa kuamka kuswali.
  4. Umuhimu wa matendo haya matatu; kwa sababu ya usia wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwausia idadi kubwa ya Maswahaba zake.
  5. Amesema bin Daqiq Al-Iid katika kauli yake: "Na rakaa mbili za Dhuha": Huenda kataja chache ambazo unapatikana msisitizo wa kuzifanya, na katika hili kuna dalili ya kuwa Dhuha ni sunna, nakuwa kwa uchache ni rakaa mbili.
  6. Wakati wa swala ya Dhuha: Ni baada ya kuchomoza Jua kwa robo saa takriban, na unakwenda wakati wake mpaka kabla ya Adhuhuri kwa dakika kumi takriban, na idadi: Kwa uchache ni rakaa mbili, na zimetofautiana kauli za wanachuoni kuhusu wingi wake; wakasema: Rakaa nane, na wakasema: Hakuna kiwango cha wingi wake.
  7. Wakati wa witiri: Baada ya swala ya Ishaa mpaka kuchomoza Alfajiri, na uchache wake ni rakaa moja, na wingi wake ni rakaa kumi na moja.
Ziada