+ -

عَنْ عَمَّارِ بنِ ياسِرٍ رضي الله عنه قال:
بَعَثَنِي رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فِي حَاجَةٍ، فَأَجْنَبْتُ فَلَمْ أَجِدِ الْمَاءَ، فَتَمَرَّغْتُ فِي الصَّعِيدِ كَمَا تَمَرَّغُ الدَّابَّةُ ثُمَّ أَتَيْتُ النَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، فَذَكَرْتُ ذَلِكَ لَهُ فَقَالَ: «إِنَّمَا كَانَ يَكْفِيكَ أَنْ تَقُولَ بِيَدَيْكَ هَكَذَا» ثُمَّ ضَرَبَ بِيَدَيْهِ الْأَرْضَ ضَرْبَةً وَاحِدَةً، ثُمَّ مَسَحَ الشِّمَالَ عَلَى الْيَمِينِ، وَظَاهِرَ كَفَّيْهِ وَوَجْهَهُ.

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 368]
المزيــد ...

Kutoka kwa Ammari Bin Yasiri radhi za Allah ziwe juu yake amesema:
Aliniagiza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika haja fulani, nikapatwa na janaba, nikawa sikupata maji, nikajigaragaza katika udongo kama anavyojigaragaza mnyama, kisha nikamuendea Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Nikamsimulia hilo, akasema: "Hakika ilikuwa inakutosheleza kupiga kwa mikono yako hivi" Kisha akapiga kwa mikono yake miwili chini ya ardhi mpigo mmoja, kisha ukapaka mkono wa kushoto juu ya mkono wa kulia, na juu ya viganja vyake na uso wake".

Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Alimtuma Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- Ammari Bin Yasiri radhi za Allah ziwe juu yake katika moja ya safari kwa baadhi ya haja zake, akapatwa na janaba kwa tendo la ndoa au kushukwa na manii kwa matamanio, na hakupata maji ili aoge, Na alikuwa hajui hukumu ya tayamam kwa ajili ya janaba, bali alikuwa anajua hukumu yake kwa hadathi ndogo, akajitahidi na akadhani kuwa kama ambavyo hufuta kwa udongo baadhi ya viungo vya udhu kwa kuondoa hadathi ndogo, akaona kuwa kutayamam kwa kuondoa janaba ni lazima aeneze udongo mwili mzima; kwa kuchukulia kipimo katika maji, akajigeuzageuza katika udogo mpaka akaueneza mwili mzima na akaswali, alipokuja kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-, akamueleza kuhusu hilo; ili aone je yeye amepatia au amekosea? Akambainishia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- namna ya kujitwaharisha kutokana na hadathi mbili, ndogo kama haja ndogo, na hadathi kubwa kama janaba: Nako ni mtu kupiga kwa mikono yake miwili juu ya udongo mpigo mmoja, kisha afute kwa mkono wa kushoto juu ya mkono wa kulia, na juu ya viganja vyake na uso wake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الغوجاراتية القيرقيزية النيبالية اليوروبا الدرية الصومالية المالاجاشية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ulazima wa kutafuta maji kabla ya kutayamam.
  2. Sheria ya kutayamam kwa mwenye janaba na akawa hakupata maji.
  3. Kutayamam kwa hadathi kubwa, ni sawa na kutayamam kwa hadathi ndogo.
Ziada