عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «قَارِبُوا وسَدِّدُوا، واعلَمُوا أَنَّه لَن يَنجُو أَحَد مِنكُم بِعَمَلِهِ» قالوا: ولا أنت يا رسول الله؟ قال: «ولاَ أَنَا إِلاَّ أَن يَتَغَمَدَنِي الله بِرَحمَة مِنْه وَفَضل».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Fanyeni matendo na muwe na msimamo, na tambueni kuwa hatosalimika mmoja wenu kwasababu ya matendo yake", wakasema: Hata wewe Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu?! Akasema: "Hata mimi isipokuwa atakaponifunika mimi Mwenyezi Mungu kwa huruma zake na fadhila zake".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Hadithi hii inaonyesha, kuwa na msimamo ni kulingana na uwezo, nayo ni kauli ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- "Fanyeni matendo na muwe na msimamo" Yaani: chungeni kupatia, Yaani: chungeni matendo yenu kuwa yako sawa na haki kwa kadiri iwezekanavyo, na hiyo; ni kwasababu mwanadamu vyovyote atakavyofikia daraja la uchamungu, ni lazima tu atakosea, mwanadamu ameamrishwa achunge matendo na awe na msimamo kwa kadiri awezavyo. kisha akasema -Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Na tambueni kuwa hatosalimika mmoja wenu kwasababu ya matendo yake" Yaani: Hatosalimika na moto kwasababu ya matendo yake, na hii ni kwasababu matendo hayawezi kufikia yale aliyoyawajibisha Mwenyezi Mungu Mtukufu katika shukurani, na yale ya wajibu kwake kwa waja wake miongoni mwa haki, lakini anamfunika Mwenyezi Mungu Mtukufu mja kwa rehema zake akamsamehe. Pindi aliposema: "hatosalimika mmoja wenu kwasababu ya matendo yake" Wakasema kumwambia: Hata wewe? Akasema: "Hata mimi" Yaani: Hivyo hivyo hata Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- hatosalimika kwasababu ya matendo yake, na akaliweka wazi hilo katika kauli yake: "Isipokuwa atakaponifunika Mwenyezi Mungu kwa rehema zitokazo kwake", Likaonyesha hilo kuwa mwanadamu vyovyote atakavyofikia daraja na cheo, yeye hatosalimika kwasababu ya matendo yake, hata Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- lau kama Mwenyezi Mungu hakumneemesha kwa kumsamehe madhambi yake yaliyotangulia na yajayo, yasingemsalimisha matendo yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Kikurdi Kireno
Kuonyesha Tarjama
Ziada