عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «مَنْ حَجَّ، فلَمْ يَرْفُثْ، وَلم يَفْسُقْ، رَجَعَ كَيَوْمَ وَلَدْتُهُ أُمُّهُ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Hurayra radhi za Allah ziwe juu yake hadithi iliyo rufaishwa kwa Mtume: (Mwenye kuhiji na akawa hakusema maneno machafu wala kutenda matendo machafu, anarudi kama siku alivyo zaliwa na mama yake (akiwa hana dhambi).
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Atakae Hiji kwaajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na yakawa hayakupatikana kwake maneno machafu, wala matendo mabaya wakati wa kutekeleza ibada, na akawa hakuleta maasi yoyote, anarudi kutoka katika Hija yake akiwa kasamehewa, kama anavyozaliwa mtoto mchanga akiwa kasalimika na madhambi, na hija kufuta madhambi ni maalumu kwa madhambi madogo tu, ama madhambi makubwa ni lazima kufanya toba.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Hija huitakasa nafsi kutokana na matendo machafu na maovu.
  2. Hija hufuta madhambi na makosa yale yaliyokuwa kabla yake.
  3. Matendo mabaya hata kama yamekatazwa katika hali zote, katazo lake linakuwa na mkazo zaidi katika Hija, kwa kuitukuza ibada ya Hija katika nyumba ya Mwenyezi Mungu tukufu.
  4. Mwanadamu huzaliwa bila makosa akiwa kaepukana na madhambi; hivyo yeye habebi makosa ya mwingine.