عن عائشة رضي الله عنها قالت: قُلتُ: يا رَسُولَ الله، نَرَى الجهادَ أفضلَ العمل، أفلا نُجاهِد؟ فقال: «لَكُنَّ أفضلُ الجهادِ: حجٌّ مبرور».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: nilisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, tunaona Jihadi kuwa ni amali bora, ni kwanini tusipigane? Akasema: "Kwenu nyinyi jihadi bora: ni hija njema"
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Alikuwa mama wa waumini Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- na wanawake wengine pamoja naye wakiitakidi kuwa amali bora kuliko zote na yenye malipo mengi zaidi ni Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu na kupambana na maadui, akawaelekeza -Ziwe juu yake sala na salamu- katika jihadi ambayo ni bora zaidi upande wao kuliko kupigana, nayo ni Hija ambayo haina madhambi yaliyo changanyika nayo, imeitwa hija kuwa ni Jihadi kwasababu ni kupambana na nafsi, na ndani yake kuna kutoa mali na nguvu za mwili.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo الدرية
Kuonyesha Tarjama