+ -

عن عبد الله بن عباس رضي الله عنهما مرفوعاً: «عمرة في رمضان تعدل حجة - أو حجة معي».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- amesema:
Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake- kumwambia mwanamke mmoja miongoni mwa Ansari (Watu wa Madina) ambaye bin Abbas alimtaja kwa jina, lakini mimi nimelisahau jina lake: "c2">“Ni nini kilikuzuia kuhiji pamoja nasi?” Akasema: Sisi tulikuwa na vilemba viwili tu, basi baba wa mwanawe na mwanawe walihiji kwa kilemba hicho na akatuachia kilemba kimoja ili tukifue.” Akasema: «Basi itakapokuja Ramadhani, basi fanya Umra, kwani Umra ndani ya Ramadhani ni sawa na Hija.”

Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, aliporejea kutoka katika Hija ya kuaga, alimwambia mwanamke mmoja wa Ansari ambaye hakuhiji: Ni nini kilikuzuia kuhiji pamoja nasi?
Akatoa udhuru kwa sababu walikuwa na ngamia wawili, hivyo mume wake na mwanawe walihiji kwa mmoja wao, na kumwacha mwingine akichota maji kisimani.
Mtume, Rehema na amani ziwe juu yake, akamwambia kuwa kufanya Umra katika mwezi wa Ramadhani ni sawa na malipo ya Hija.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Thai Kiassam السويدية الأمهرية الغوجاراتية القيرقيزية اليوروبا الدرية الصومالية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Fadhila za Umra ndani ya mwezi wa Ramadhani.
  2. Umra ndani ya Ramadhani inalingana sawa na Hija katika malipo, haina maana ya kuondosha uwajibu wa Hija.
  3. Malipo ya matendo huzidi kulingana na utukufu wa nyakati, ikiwemo matendo yanayofanywa ndani ya Ramadhani.