عن عَمْرُو بْنُ عَامِرٍ عَنْ ‌أَنَس بن مالك قَالَ:
كَانَ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَتَوَضَّأُ عِنْدَ كُلِّ صَلَاةٍ، قُلْتُ: كَيْفَ كُنْتُمْ تَصْنَعُونَ؟ قَالَ: يُجْزِئُ أَحَدَنَا الْوُضُوءُ مَا لَمْ يُحْدِثْ.

[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 214]
المزيــد ...

Kutoka kwa Amri bin Aamiri kutoka kwa Anasi amesema:
Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akitawadha kila wakati wa swala, nikasema: Nyinyi mlikuwa mnafanya vipi? Akasema: Ulikuwa ukimtosha mmoja wetu udhu mmoja madam hajatengukwa.

[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [Swahiih Al Bukhaariy - 214]

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akitawadha kwa kila swala ya faradhi hata kama hajatengukwa udhu; Na hii ni kwa sababu ya kupata malipo na fadhila.
Na inafaa kwa mtu kuswali kwa zaidi ya swala moja kwa udhu mmoja madam bado yuko na udhu wake.

Katika Faida za Hadithi

  1. Mwenendo uliodumu zaidi wa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- ni kushika udhu kwa kila swala; ili kutaka ukamilifu zaidi.
  2. Sunna ya kushika udhu kila wakati wa swala.
  3. Inafaa kutekeleza zaidi ya swala moja kwa udhu mmoja.
Kuonyesha Tarjama
Lugha: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Ziada (58)