عن عَمْرُو بْنُ عَامِرٍ عَنْ ‌أَنَس بن مالك قَالَ:
كَانَ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَتَوَضَّأُ عِنْدَ كُلِّ صَلَاةٍ، قُلْتُ: كَيْفَ كُنْتُمْ تَصْنَعُونَ؟ قَالَ: يُجْزِئُ أَحَدَنَا الْوُضُوءُ مَا لَمْ يُحْدِثْ.

[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Amri bin Aamiri kutoka kwa Anasi amesema:
Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akitawadha kila wakati wa swala, nikasema: Nyinyi mlikuwa mnafanya vipi? Akasema: Ulikuwa ukimtosha mmoja wetu udhu mmoja madam hajatengukwa.

Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akitawadha kwa kila swala ya faradhi hata kama hajatengukwa udhu; Na hii ni kwa sababu ya kupata malipo na fadhila.
Na inafaa kwa mtu kuswali kwa zaidi ya swala moja kwa udhu mmoja madam bado yuko na udhu wake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Mwenendo uliodumu zaidi wa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- ni kushika udhu kwa kila swala; ili kutaka ukamilifu zaidi.
  2. Sunna ya kushika udhu kila wakati wa swala.
  3. Inafaa kutekeleza zaidi ya swala moja kwa udhu mmoja.