عن أبي هريرة رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم : "لاَ يَقْبَل الله صلاَة أَحَدِكُم إِذا أَحْدَث حَتَّى يَتوضَّأ".
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: Amesema Mtume Rehema na Amani zimfikie: "Haikubali Mwenyezi Mungu swala ya mmoja wenu atakapotengukwa udhu mpaka atawadhe".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Sheria tukufu imemuelekeza Mwenye kutaka kuswali, asiingie kusali ispokuwa anapokuwa katika hali nzuri na muonekano mzuri, kwasababu ndio kiunganishi kizito kati ya mja na Mola wake, na ndio njia ya kuelekea kuzungumza naye, hivyo ameamrisha kutia udhu na kufanya usafi, na akamueleza kuwa swala inakataliwa na wala haikubaliwi pasina kuwa na twahara.