عَنِ ‌ابْنِ عَبَّاسٍ رضي الله عنهما قَالَ:
تَوَضَّأَ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ مَرَّةً مَرَّةً.

[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Imepokewa kutoka kwa Bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- amesema:
Alitawadha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- mara moja moja.

Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- katika baadhi ya nyakati zake anapotawadha anaosha kila kiungo katika viungo vya udhu mara moja moja, anaosha uso pamoja kusukutua na kupandisha maji puani, na mikono miwili na miguu miwili mara moja moja, na hiki ndicho kiwango cha wajibu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kilicho wajibu katika kuosha viungo ni mara moja moja, inayozidi inapendeza kufanya hivyo.
  2. Sheria ya kutia udhu mara moja moja katika baadhi ya nyakati.
  3. Sheria katika kufuta kichwa ni mara moja.