عن عبد الله بن عمرو رضي الله عنهما عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «من قَتَلَ مُعَاهَدًا لم يَرَحْ رَائحَةَ الجنة، وإن رِيْحَهَا تُوجَدُ من مَسِيرَة أربعين عامًا».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillahi bin Amri- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Atakayemuua aliyechukua ahadi ya kulindwa, hatonusa harufu ya pepo, na hakika hurufu yake hupatikana kuanzia mwendo wa miaka arobaini".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Imejulisha hadithi kuwa atakaye muua aliyechukua ahadi ya kulindwa bila haki, na mtu huyu ni yule aliyeingia ardhi ya kiislamu kwa ahadi na amani, au akawa ni katika watu waliopewa hifadhi, katika makafiri, Mwenyezi Mungu hatomuwezesha kuingia peponi, na hakika harufu yake hupatikana kuanzia masafa ya miaka arobaini, na hii ni dalili juu ya umbali wake na hiyo pepo, nayo inaonyesha pupa ya uislamu juu ya kuhifadhi damu isiyokuwa na hatia miongoni mwa wanaochukua ahadi ya kulindwa na wanaopewa hifadhi, nakuwa kuwauwa bila hatia ni katika madhambi makubwa.