عن عبد الله بن عمرو رضي الله عنهما عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «من قَتَلَ مُعَاهَدًا لم يَرَحْ رَائحَةَ الجنة، وإن رِيْحَهَا تُوجَدُ من مَسِيرَة أربعين عامًا».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillahi bin Amri- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Atakayemuua aliyechukua ahadi ya kulindwa, hatonusa harufu ya pepo, na hakika hurufu yake hupatikana kuanzia mwendo wa miaka arobaini".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Imejulisha hadithi kuwa atakaye muua aliyechukua ahadi ya kulindwa bila haki, na mtu huyu ni yule aliyeingia ardhi ya kiislamu kwa ahadi na amani, au akawa ni katika watu waliopewa hifadhi, katika makafiri, Mwenyezi Mungu hatomuwezesha kuingia peponi, na hakika harufu yake hupatikana kuanzia masafa ya miaka arobaini, na hii ni dalili juu ya umbali wake na hiyo pepo, nayo inaonyesha pupa ya uislamu juu ya kuhifadhi damu isiyokuwa na hatia miongoni mwa wanaochukua ahadi ya kulindwa na wanaopewa hifadhi, nakuwa kuwauwa bila hatia ni katika madhambi makubwa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Uharamu wa kumuua aliyechukua ahadi ya kulindwa,nakuwa hilo ni dhambi kubwa miongoni mwa madhambi makubwa; kwasababu amempangia kunyimwa kuingia peponi kwa muonekano wa hadithi.
  2. Imekuja katika baadhi ya riwaya za hadithi kuwa muuwaji "Bila hatia" na "bila haki" na kubaguliwa huku kunafahamika katika kanuni za sheria.
  3. Ulazima wa kutimiza makubaliano.
  4. Kuthibitishwa kuwa pepo ina harufu.
  5. Nikuwa harufu ya pepo hupatikana kuanzia masafa ya mbali.
Ziada