عن أبي ثَعْلبة الخُشني رضي الله عنه قال: «أَتَيْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم فقلت: يا رسول الله، إنا بأرض قوم أهل كتاب، أَفَنَأْكُلُ في آنِيَتِهِم؟ وفي أرض صيد، أَصِيدُ بِقَوْسِي وبِكَلْبِي الذي ليس بِمُعَلَّمٍ، وبِكَلْبِي المُعَلَّمِ، فما يَصلح لي؟ قال: أمَّا مَا ذَكَرْتَ- يعني من آنية أهل الكتاب-: فإِنْ وجدْتُمْ غيرها فلا تأكلوا فيها، وإِنْ لم تَجِدُوا فاغسِلوهَا، وكلوا فِيهَا، وما صدتَ بِقَوْسِكَ، فذَكَرْتَ اسمَ الله عَلَيه فَكُلْ، وما صِدْتَ بِكَلْبِكَ المُعَلَّمِ، فَذَكَرْتَ اسْمَ الله عليه فَكُلْ، وما صِدْتَ بِكَلْبِكَ غيرِ المُعَلَّمِ فَأَدْرَكْتَ ذَكَاتَهُ فَكُلْ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Tha'laba Al-khushaniy- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: "Nilimuendea Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Nikasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Hakika sisi tuko katika ardhi ya watu wa kitabu, je tule katika vyombo vyao? na katika ardhi ya mawindo, ninawinda kwa upinde wangu na kwa mbwa wangu ambaye hajafunzwa, na kwa mbwa aliyefunzwa, ni kipi kinachofaa kwangu? Akasema: Ama ulichokisema- yaani kuhusu vyombo vya watu wa kitabu- : mkipata vyombo vingine basi msile katika vyombo hivyo, msipopata vingine basi viosheni, na kuleni ndani yake, na ulichokiwinda kwa upinde wako, ukataja jina la Mwenyezi Mungu juu yake basi kula, na ulichokiwinda kwa mbwa wako aliyefunzwa, na ukataja jina la Mwenyezi Mungu juu yake basi kula, na ulichowinda kwa mbwa wako ambaye hajafunzwa ukaweza kukichinja basi kula".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Alieleza Abuu Thaalaba -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- yakuwa wao wamepewa mtihani wa ujirani wa watu wa kitabu, na makusudio ya hao ni mayahudi na wakristo, je ni halali kwao wale katika vyombo vyao pamoja na dhana ya unajisi wake? Akamjibu kuwa inafaa kula ndani yake, Na ni bora zaidi kuvitumia katika matumizi yasiyokuwa kula kwa sharti mbili: 1- Kutopatikana vyombo vingine tofauti na hivyo. 2- Na wavioshe. Na akamueleza kuwa wao wako katika ardhi ya mawindo, nakuwa yeye anawinda kwa upinde wake na kwa mbwa wake aliyefunzwa juu ya uwindaji na adabu zake, na kwa mbwa wake ambaye hajafunzwa, ni kipi kinachofaa kwake na cha halali katika viwindwa vya hivi vifaa? Akamjibu kuwa alivyoviwinda kwa upinde wake basi hivyo ni halali, kwa sharti ataje jina la Mwenyezi Mungu -Mtukufu- wakati wa kurusha mshale. Na ama unavyoviwinda kwa mbwa, wakiwa wamefunzwa na ukataja jina la Mwenyezi Mungu wakati wa kumtuma hicho ni halali pia, na ama ambao hawajafunzwa, si halali viwindwa vyake isipokuwa atakapokikuta mtu kikiwa hai na akichinje kichinjo cha kisheria.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kichina Kifursi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo
Kuonyesha Tarjama
Ziada