عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «يَعْقِدُ الشيطان على قَافِيَةِ رأسِ أحدِكم، إذا هو نام، ثلاث عُقَدٍ، يَضْرِب على كل عُقْدَةٍ: عليك لَيلٌ طويل فَارْقُدْ، فإن استيقظ، فذكر الله تعالى انحَلَّتْ عُقْدَةٌ، فإن تَوضِّأ، انْحَلّتْ عُقدَةٌ، فإن صلى، انْحَلَّتْ عُقَدُهُ كُلُّها، فأصبح نشيطا طَيِّبَ النفس، وإلا أصبح خَبِيثَ النَّفْس كَسْلَان».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Anafunga shetani juu ya kisogo cha kichwa cha mmoja wenu, pindi anapolala, mafundo matatu, anapiga katika kila fundo: Unatakiwa kulala usiku mrefu basi lala, pindi anapoamka na akamtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu linafunguka fundo moja, akitawadha, linafunguka fundo jingine, na akiswali, yanafunguka mafundo yake yote, anaamka akiwa na uchangamfu na moyo mkunjufu, na vinginevyo basi anaamka akiwa na nafsi chafu tena mvivu".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Maana ya hadithi: Nikuwa anafunga shetani kisogoni mwa kila mtu aliyelala mafundo matatu, Na fundo: Linakuwa katika uhalisia wake na kwamba alikuwa akimfungia mchawi yule anayemroga anachukua kamba anafunga fundo katika kamba hiyo kisha anazungumza hapo maneno ya kiuchawi, basi kwa hilo anaathirika yule aliyerogwa, na katika riwaya ya bin Majah: "Anafunga katika kisogo cha mmoja wenu nyakati za usiku kamba ikiwa na mafundo matatu "Bali anafunga mwisho wa kichwa pekee; kwasababu ndio kituo cha nguvu, na ndio nafasi ya harakati, nayo ni sehemu inayokubali haraka sana kwa shetani na ni nyepesi mno kuitikia anapoihitaji, anapoifunga basi anapata uwezo wa kuimiliki roho ya mwanadamu, na kuijazia usingizi. "Anapiga katika kila fundo", Yaani anapiga kwa mkono wake ikiwa ni kuhakikisha na kuthibitisha sehemu ya kila fundo alilolifunga, kwa kauli hii nayo ni: "Unatakiwa kulala usiku mrefu" Yaani: ubaki umesinzia muda mrefu usiku, lala upendavyo, kwani muda wowote utakapoamka utapata muda wa kutosha kutekeleza swala za usiku, "Basi lala": Yaani: rudi katika usingizi wako. "Basi anapoamka na akamtaja Mwenyezi Mungu linafunguka fundo moja" kwasababu ya kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu, "Akitawadha linafunguka fundo" Yaani: fundo la pili kwasababu ya baraka za udhu, Na katika riwaya ya Muslim: "Akitawadha yanafunguka mafundo mawili". Na inakusanya pia pale atakapooga kwaajili ya kujitwaharisha kutokana hadathi kubwa (kama janaba). "Akiswali" "Hata rakaa moja" yanafunguka mafundo yake" linafunguka fundo la tatu, na katika riwaya ya Bukhariy "Yanafunguka mafundo yake yote" "Anakuwa na uchangamfu" kwa furaha yake kwa kile alichomfanyia Mwenyezi Mungu katika msaada wa kufanya ibada na yale aliyoyaahidi miongoni mwa malipo na yale yaliyomuondokea miongoni mwa mafundo ya shetani. "Akiwa na moyo mkunjufu" kwa yale aliyombariki Mwenyezi Mungu katika nafsi yake kwa harakati hizi nzuri "Na vinginevyo" Yaani: Na ikiwa hatofanya haya yaliyotajwa katika mambo matatu "Anaamka akiwa na nafsi chafu tena mvivu" Yaani: hali yake ikiwa imebadilika; kwasababu ya usaliti wa shetani kwake kwa yale aliyokuwa ameyazoea au ameyanuia katika mambo ya kheri. Amesema Al Hafidh Ibni Hajar -Mwenyezi Mungu amrehemu- Na kinachoonekana wazi nikuwa, katika swala za usiku kuna siri katika kuisafisha nafsi hata kama mwenye kuswali hatohisi chochote miongoni mwa hayo yaliyotajwa, na hivyo hivyo kinyume chake, na katika hilo kuna ishara kutoka katika kauli yake Mtukufu: "Hakika kuamka usiku (na kufanya ibada) kunawafikiana zaidi na moyo na maneno (yake) yanatua zaidi" mwisho wa kunukuu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama