+ -

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضيَ اللهُ عنه أَنَّ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، قَالَ:
«أَحَبُّ الْبِلَادِ إِلَى اللهِ مَسَاجِدُهَا، وَأَبْغَضُ الْبِلَادِ إِلَى اللهِ أَسْوَاقُهَا».

[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 671]
المزيــد ...

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- amesema:
"Miji inayopendeka zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni misikiti yake, na miji inayochukiwa zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni masoko yake".

[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 671]

Ufafanuzi

Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa sehemu zinazopendeka zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni misikiti yake; kwa sababu ni nyumba za ibada, na zimeasisiwa kwa uchamungu, na miji inayochukiza zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni masoko yake; kwa sababu masoko mara nyingi ndio kitovu cha ghushi na udanganyifu na riba na viapo vya uongo, na kwenda kinyume na ahadi, na kupuuza kumtaja Mwenyezi Mungu.

Katika Faida za Hadithi

  1. Utukufu wa misikiti na heshima yake; kwa sababu ni nyumba ambazo hutajwa ndani yake jina la Mwenyezi Mungu kwa wingi.
  2. Himizo la kudumu kuwa msikitini, na wingi kwenda ndani yake, kwa kutafuta mapenzi ya Mwenyezi Mungu Mtukufu na radhi zake, na kupunguza kuzunguka masokoni, isipokuwa kwa haja maalumu; kwa kujiepusha kuingia katika sababu za hasira ya Mwenyezi Mungu.
  3. Amesema Nawawi: Misikiti ni mahali pa kushuka rehema na masoko ni kinyume chake.
Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kikurdi Kihausa Kiassam الرومانية المجرية الجورجية
Kuonyesha Tarjama
Ziada