عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «من صَام رمضان إيِمَانًا واحْتِسَابًا، غُفِر له ما تَقدَّم من ذَنْبِه».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Hadithi Marfu'u: "Atakayefunga ramadhani kwa imani na kwa kutaraji malipo, atasamehewa yaliyotangulia katika madhambi yake".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Maana ya hadithi: Nikuwa atakayefunga mwezi wa ramadhani kwa kumuamini Mwenyezi Mungu na kwa kusadikisha ahadi zake na kwa kutaraji malipo yake na kwa kukusudia radhi za Mwenyezi Mungu Mtukufu, si kwa kujionyesha wala kutaka kusikika, atasamehewa yaliyotangulia katika madhambi yake.