عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «قال الله عز وجل : كلُّ عَمَل ابن آدَم له إلا الصيام، فإنه لي وأنا أجْزِي به، والصيام جُنَّة، فإذا كان يوم صوم أحدِكُم فلا يَرْفُثْ ولا يَصْخَبْ فإن سَابَّهُ أحَدٌ أو قَاتَلَهُ فليَقل: إنِّي صائم، والذي نفس محمد بيده لَخُلُوفُ فَمِ الصَّائِم أطيب عند الله من رِيحِ المِسْكِ، للصائم فرحتان يَفْرَحُهُمَا: إذا أفطر فَرِح بفطره، وإذا لَقِي ربَّه فَرِح بِصَوْمه». وهذا لفظ رواية البخاري. وفي رواية له: «يَتْرُك طَعَامه، وشَرَابه، وشَهوته من أجلي، الصيام لي وأنا أَجْزِي به، والحسنة بعشر أمثالها». وفي رواية لمسلم: «كلُّ عَمَل ابن آدم يُضَاعَف، الحَسَنة بِعَشر أمْثَالها إلى سَبْعِمِئَة ضِعْف، قال الله تعالى: إلا الصَّوم فإنه لي وأنا أجْزِي به؛ يَدَع شَهَوته وطَعَامه من أجلي، للصائم فرحتان: فَرْحَة عند فِطْره، وفَرْحَة عند لقِاء ربِّه، ولَخُلُوف فيه أطْيَب عند الله من رِيحِ المِسْكِ».
[صحيح] - [الرواية الأولى: متفق عليها. الرواية الثانية: رواها البخاري. الرواية الثالثة: رواها مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Amesema Mwenyezi Mungu -Aliyetakasika na kutukuka-: Kila amali ya mwanadamu hiyo ni ya kwake isipokuwa swaumu, bila shaka hiyo ni yakwangu na mimi ndiye ninayeilipa, na funga ni kinga, itakapokuwa ni siku ya kufunga mmoja wenu, basi asifanye mambo machafu, na wala asifanye vurugu, ikiwa mtu atamtukana au kumpiga basi na aseme: Hakika mimi nimefunga, Namuapa yule ambaye nafsi ya Muhammadi iko mkononi mwake hakika harufu ya kinywa cha mtu aliyefunga ni nzuri zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko hata harufu ya miski, mfungaji ana furaha mbili anazozifurahia: Anapofuturu hufurahia kufuturu kwake, na atakapokutana na Mola wake atafurahia swaumu yake". Na hili ni tamko la riwaya ya Bukhariy. Na riwaya nyingine ya kwake: "Anaacha chakula chake na kinywaji chake, na matamanio yake kwaajili yangu, swaumu ni yangu na mimi ndiye ninayeilipa, na jema moja ni sawa na mema kumi mfano wake". Na katika riwaya ya Muslim: "kila amali ya mwanadamu hulipwa mara dufu, jema moja ni sawa na mema kumi mfano wake mpaka inafika zaidi ya mia saba, amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Isipokuwa swaumu hakika hiyo ni yangu na mimi ndiye ninayeilipa; anaacha matamanio yake na chakula chake kwaajili yangu, mfungaji anafuraha mbili: furaha wakati kufuturu kwake, na furaha wakati wa kukutana kwake na Mola wake, na harufu mbaya ya kinywa chake ni nzuri sana mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko hata harufu ya miski".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika hadithil qudsiy: kuwa matendo yote mema kuanzia kauli na matendo, ya wazi na ya siri, sawa sawa yale yanahusiana na haki ya Mwenyezi Mungu, au haki za waja huzidishwa mara dufu mpaka mara sabini. Na hili ni jambo kubwa katika yale yanayoonyesha upana wa fadhila za Mwenyezi Mungu, na wema wake kwa waja wake waumini, pale alipofanya makosa yao na uhalifu wao kuwa kosa moja malipo mara moja. Na msamaha wa Mwenyezi Mungu uko katika kosa hilo. Na akaondoa katika hadithi hii malipo ya swaumu, kwani mfungaji anapewa malipo yake bila ya hesabu, yaani nikuwa yeye anazidishiwa ziada nyingi; kwasababu swaumu imekusanya aina tatu za subira, ndani yake: kuna kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu na kusubiri kutokumuasi Mwenyezi Mungu na kusubiri juu ya mipango ya Mwenyezi Mungu. Ama kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu, ni kwasababu mwanadamu anailazimisha nafsi yake juu ya kufunga pamoja nakuwa inachukia wakati mwingine kwasababu ya kupata kwake tabu, si kwasababu Mwenyezi Mungu ameifaradhisha, na lau kama mtu ataichukia swaumu kwasababu Mwenyezi Mungu ameifaradhisha basi yangeporomoka matendo yake, lakini amechukia tu zile tabu zake, lakini pamoja na hivyo anailazimisha nafsi yake juu ya hilo akasubiri kuto kula na kunywa nakufanya tendo la ndoa kwaajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kwaajili hii kasema Mwenyezi Mungu Mtukufu katika hadithil qudsiy: Anaacha chakula chake na kinywaji chake na matamanio yake kwaajili yangu. Aina ya pili miongoni mwa aina za subira: Ni kusubiri kutokumuasi Mwenyezi Mungu, na hili linapatikana kwa mfungaji kwasababu yeye anaisubirisha nafsi yake kutokumuasi Mwenyezi Mungu Mtukufu akayaepuka mambo ya kipuuzi na machafu na uongo na mengineyo katika maharamisho ya Mwenyezi Mungu. Ya tatu: Ni kusubiri juu ya makadirio ya Mwenyezi Mungu, na hii ni kwasababu mtu hupatwa katika siku za kufunga, na hasa hasa katika siku zenye joto kali na ndefu uvivu na uchovu na kiu na yale yanayomuumiza na yakamuudhi lakini yeye anavumilia; kwa kutaraji radhi za Mwenyezi Mungu Mtukufu. Baada ya kuwa swaumu imekusanya aina hizi tatu za subira ikawa malipo yake hayana hesabu, Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Hakika hutimiziwa wenye kusubiri malipo yao bila ya hesabu). Na imeonyesha hadithi kuwa swaumu iliyokamili ni ile ambayo mja ndani yake anaacha mambo mawili: Yale yenye kufunguza yanayoonekana, kama chakula kinywaji tendo la ndoa na yenye kuambatana na hayo. Na makosa ya kimatendo, kama kufanya uchafu na ugomvi na kusema uongo na maasi yote, na ugomvi na mizozo inayoleta chuki, na kwasababu hii alisema: "Basi na asifanye uchafu": Yaani asizungumze maneno machafu "Na asifanye fujo": kwa maneno yenye kuleta fitina na ugomvi, atakayeyatimiza mambo haya mawili: Kuacha yenye kufunguza, na kuacha maharamisho, yatakuwa yametimia kwake malipo ya wafungaji, na asiyefanya hivyo yatapungua malipo ya swaumu yake kwasababu ya kukithiri makosa haya, kisha akamuelekeza mfungaji katika hali ambayo ikiwa atatukanwa au kumgombezwa na mtu basi aseme kumwambia kwa ulimi wake: "Mimi nimefunga". Yaani asimrudushie matusi yake, bali amueleze kuwa yeye amefunga, anamwambia hivyo ili asijekupanda kiburi huyu aliyemtukana, kama akisema: mimi sishindwi kupambana na wewe, lakini mimi nimefunga, ninaiheshimu swaumu yangu na ninachunga kukamilika kwake, na ameamrisha Mwenyezi Mungu na Mtume wake, Na kauli yake: "swaumu ni kinga" Yaani ni kinga anayoitumia mja kuyaepuka madhambi katika dunia na anajizoesha nayo katika mambo ya kheri, na ni kinga ya adhabu. "Mfungaji anafuraha mbili: furaha wakati wa kufuturu kwake, na furaha wakati wa kukutana na Mola wake". Hizi ni thawabu mbili: ya haraka, na ya baadaye. Ya haraka: Inaonekana, anapofuturu mfungaji hufurahia neema ya Mwenyezi Mungu juu yake kwa kukamilisha swaumu, na amefurahi kwa kupata matamanio yake yale aliyozuiwa mchana. Na ya baadaye: ni furaha wakati wa kukutana na Mola wake kwa radhi zake na ukarimu wake, na furaha hii ya haraka ni dondoo ya hiyo ya baadaye, nakuwa Mwenyezi Mungu atazikusanya furaha hizo zote kwa mfungaji. Kisha akaapa -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa Mola wake ambaye nafsi yake iko mkononi mwake kuwa harufu ya kinywa cha mfungaji ni nzuri zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko harufu ya miski", na katika riwaya ya Muslim: "Ni nzuri zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu siku ya kiyama" Atamlipa Mwenyezi Mungu Mtukufu siku ya kiyama kwa kuisafisha harufu yake hiyo mbaya duniani mpaka iwe mfano wa harufu nzuri kuliko harufu ya miski.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kireno
Kuonyesha Tarjama