عَنْ عَائِشَةَ أُمِّ المؤْمنينَ رَضيَ اللهُ عنها:
أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ كَانَ إِذَا خَرَجَ مِنَ الغَائِطِ قَالَ: «غُفْرَانَكَ».

[صحيح] - [رواه أبو داود والترمذي وابن ماجه وأحمد] - [سنن أبي داود: 30]
المزيــد ...

Imenukuliwa kutoka kwa Aisha mama wa waumini radhi za Allah ziwe juu yake:
Yakwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake alikuwa anapotoka kukidhi haja anasema: "Ghufraanaka" Msamaha unatoka kwako.

[Sahihi] - [Imepokelewa na Abu Daud, Tirmidhiy, Ibn Majah na Ahmad] - [Sunanu Abii Daud - 30]

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake anapotoka kukidhi haja yake msalani anasema: " Ninakuomba (Msamaha) Ewe Mwenyezi Mungu.

Katika Faida za Hadithi

  1. Ni sunna kusema: "Ghufraanaka" baada ya kutoka mahala pa kukidhi haja.
  2. Mtume rehema na amani ziwe juu yake kumtaka msamaha Mola wake katika hali zake zote.
  3. Inasemekana katika sababu ya kuomba msamaha baada ya kukidhi haja ni kwa sababu ya uzembe wa kushukuru neema nyingi za Mwenyezi Mungu, ikiwemo kurahisishiwa kutoka kile kinachokuudhi, na ninaomba msamaha wako kwa kushughulishwa na kukidhi haja nikaacha kukutaja.
Kuonyesha Tarjama
Lugha: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Ziada (50)