عَنْ سَلْمَانَ رَضيَ اللهُ عنه قَالَ:
قَالَ لَنَا الْمُشْرِكُونَ: إِنِّي أَرَى صَاحِبَكُمْ يُعَلِّمُكُمْ حَتَّى يُعَلِّمَكُمُ الْخِرَاءَةَ، فَقَالَ: أَجَلْ، إِنَّهُ نَهَانَا أَنْ يَسْتَنْجِيَ أَحَدُنَا بِيَمِينِهِ، أَوْ يَسْتَقْبِلَ الْقِبْلَةَ، وَنَهَى عَنِ الرَّوْثِ وَالْعِظَامِ وَقَالَ: «لَا يَسْتَنْجِي أَحَدُكُمْ بِدُونِ ثَلَاثَةِ أَحْجَارٍ».
[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 262]
المزيــد ...
Kutoka kwa Salman radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake amesema:
Washirikina walisema kutuambia: Hakika mimi ninamuona jamaa yenu anakufundisheni kila kitu, mpaka anakufundisheni kukidhi haja, akasema: Ndiyo, hakika yeye ametukataza kustanji mmoja wetu kwa mkono wake wa kulia, au kuelekea kibla, na akakataza kinyesi cha wanyama na mifupa, na akasema: "Asistanji mmoja wenu kwa chini ya mawe matatu".
[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 262]
Amesema Salman Al-Faarisi radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: Washirikina walisema kwa kutukejeli: Hakika Nabii wenu anakufundisheni kila kitu, mpaka anakufundisheni namna gani mtakidhi haja zenu kama haja ndogo au kubwa! Akasema Salmaan: Ndiyo, ametufundisha adabu za kukidhi haja; na miongoni mwake ni kwamba alitukataza rehema na amani ziwe juu yake kustanjia baada ya kukidhi haja kwa mkono wa kulia, kwa kuulinda na najisi na kwa kuupa heshima, au kuelekea kibla wakati wa haja ndogo au kubwa, na akakataza kustanji kwa kinyesi cha wanyama na mabaki yake na mifupa yake, na asitosheke aliyekidhi haja katika kustanji kwa chini ya mawe matatu.