عن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه قال: «سُئِلَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم عَنْ الرَّجُلِ: يُقَاتِلُ شَجَاعَةً، وَيُقَاتِلُ حَمِيَّةً، وَيُقَاتِلُ رِيَاءً، أَيُّ ذَلِكَ فِي سَبِيلِ الله؟ فَقَالَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : مَنْ قَاتَلَ لِتَكُونَ كَلِمَةُ الله هِيَ الْعُلْيَا، فَهُوَ فِي سَبِيلِ الله».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Musa Radhi za Allah ziwe juu yake amesema:
Aliulizwa Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake kuhusu mtu anayepigana kwa kutaka kuonekana jasiri, na anayepigana kwa hamasa za ukabila, au anayepigana kwa kutaka kuonekana. Ni yupi kati ya hao anayepigana kwa ajili ya Mwenyezi Mungu? Akasema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake: “Mwenye kupigana ili neno la Mwenyezi Mungu liwe juu, basi huyo yuko katika Njia ya Mwenyezi Mungu."
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Mtume rehema na amani ziwe juu yake aliulizwa kuhusu kutofautiana kwa malengo ya wapiganaji hao; mwenye kupigana kwa kutaka kuonekana jasiri, au kwa hamasa, au ionekane nafasi yake kati ya watu, au mengineyo, ni lipi kati ya haya lipo kwa ajili ya Allah? Akaeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa mpiganaji katika njia ya Mwenyezi Mungu ni yule anayepigana ili neno la Mwenyezi Mungu liwe juu.