عن أبي سعيد الخدري رضي الله عنه أن رسول الله -صلى الله وعليه وسلم- قال: «لا ضَرَرَ ولا ضِرَارَ».
[صحيح] - [رواه ابن ماجه من حديث أبي سعيد الخدري -رضي الله عنه- ومن حديث عبادة بن الصامت -رضي الله عنه-. ورواه أحمد من حديث عبادة بن الصامت -رضي الله عنه-. ورواه مالك من حديث عمرو بن يحي المازني مرسلا]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abii Saidi Al-Khudriy- Radhi za Allah ziwe juu yake- Yakwamba Mtume -Rehma na amani ziwe juu yake- "Amesema: "Hakufai kujidhuru wala kumdhuru mwingine.".
Sahihi - Imepokelewa na Ibnu Maajah

Ufafanuzi

Hadithi hii inatupa kanuni ya uislamu katika sheria, na kanuni za tabia njema na namna ya kuamiliana na watu, nayo ni kuwaondolea madhara kwa aina zake tofauti tofauti na njia zake, madhara yameharamishwa na kuondoa madhara ni wajibu, na madhara bado yanaendelea kudhuru, na madhara yameharamishwa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Mtume kapewa kufupisha maneno, na ushahidi wa hili ni mwingi, nalo ni katika mambo aliyopendelewa -Ziwe juu yake Rehema na Amani-.
  2. Madhara huondolewa.
  3. Kukatazwa kulipiza zaidi ya jinsi mtu alivyofanyiwa.
  4. Hakuwaamrisha Mwenyezi Mungu waja waje kufanya kitu kinachowadhuru.
  5. Kuja kwa kanusho inamaana ya katazo.
  6. Kuharamishwa kuanzisha madhara kwa kauli au kwa vitendo au kwa kuacha.
  7. Dini ya uislamu ndiyo dini ya Amani.
  8. Hadithi hii inazingatiwa kuwa ni msingi katika misingi ya sheria, nayo nikuwa sheria haikubali kuanzisha madhara, lakini pia haipingi madhara kuhama kwenda kwa mtu mwingine.
  9. Je kati ya kudhuru na kuanzisha madhara kuna tofauti au la? Wapo waliyosema: yote mawili maana yake ni moja ispokuwa imekuja kama msisitizo, na kauli maarufu nikuwa kati yake kuna tofauti, nikuwa madhara ni jina, na kudhuru ni kitendo, maana yake nikuwa madhara yamekanushwa katika sheria, na kuingiza madhara bila sababu pia, na yasemekana: madhara ni mtu kumpatia mwenzie madhara kwa yale atakayonufaika nayo yeye, na kuhamisha madhara: ni mtu kumuingizia madhara mwingine bila ya yeye kunufaika nayo, kama atakayekataza mambo ambayo hayamdhuru yeye lakini anayedhurika ni yule mwenye kukatazwa, na wameipa nguvu kauli hii kundi katika wanachuoni, miongoni mwao ni Ibn Abdil Barri na Ibn Swalah, na yasemekana: Kudhuru: Ni mtu kumdhuru ambaye asiyemdhuru: kuanzisha madhara: ni amdhuru yule ambaye tayari alimdhuru kwa namna ambayo haifai kisheria, na kwa namna yoyote ile Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake amekataza kudhuru na kuhamisha madhara bila sababu za msingi.