عَنِ ابنِ مَسعُودٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«لَا يَحِلُّ دَمُ امْرِئٍ مُسْلِمٍ إِلَّا بِإِحْدَى ثَلَاثٍ: الثَّيِّبُ الزَّانِي، وَالنَّفْسُ بِالنَّفْسِ، وَالتَّارِكُ لِدِينِهِ المُفَارِقُ لِلْجَمَاعَةِ».
[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 1676]
المزيــد ...
Kutoka kwa bin Mas'udi radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake-:
"Si halali damu ya muislamu isipokuwa kwa moja kati ya mambo matatu: Mzinifu aliyeoa, na nafsi kwa nafsi, na mwenye kuacha dini yake mwenye kusambaratisha umoja".
[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح مسلم - 1676]
Amebainisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa damu ya Muislamu ni haramu, isipokuwa akifanya moja katika mambo matatu: La kwanza: Akatakayetumbukia katika uchafu wa zinaa, na hali yakuwa ameoa ndoa sahihi ya kisheria; ni halali kumuua kwa mpiga mawe. La pili: Atakayeua nafsi isiyo na hatia kwa makusudi pasina haki, atauwawa kwa sharti zake. La tatu: Mwenye kutoka katika umoja wa Waislamu; ima kwa kuacha dini yake ya Uislamu yote kwa kuritadi, au mwenye kutoka bila kuritadi kwa kuacha sehemu ya dini kama waasi, na vibaka, na wanaopiga vita Waislamu kama Makhawariji na wengineo.