عن يحيى المازني رحمه الله قال: ((شَهِدتُّ عمرو بن أبي حسن سأل عبد الله بن زيد عن وُضوء النبي صلى الله عليه وسلم ؟ فدعا بتَور من ماء، فتوضَّأ لهم وُضُوء رسول الله صلى الله عليه وسلم ، فأكفَأ على يديه من التَّورِ، فغسَل يديه ثلاثًا، ثم أدخل يدهُ في التور، فمَضْمَض واسْتَنْشَق واسْتَنْثَر ثلاثا بثلاثِ غَرَفَات، ثم أدخل يده فغسل وجهه ثلاثا، ثم أدخل يده في التور، فغَسَلَهُما مرَّتين إلى المِرْفَقَين، ثم أدخل يدَه في التَّور، فمَسَح رأسَه، فأَقْبَل بهما وأَدْبَر مرَّة واحدة، ثم غَسَل رِجلَيه)). وفي رواية: ((بدأ بمُقَدَّم رأسه، حتى ذَهَب بهما إلى قَفَاه، ثم رَدَّهُما حتَّى رَجَع إلى المكان الذي بدأ منه)). وفي رواية ((أتانا رسول الله صلى الله عليه وسلم فأخْرَجنا له ماء في تَورٍ من صُفْرٍ)).
[صحيح] - [الرواية الأولى: متفق عليها الرواية الثانية: متفق عليها الرواية الثالثة : رواها البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Yahya Al Maaziniy -Mwenyezi Mungu amrehemu- Amesema: (Nilimshuhudia Amru bin Abii Hasan alimuuliza Abdallah bin Zaidi kuhusu udhu wa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akaagiza bakuli la maji, akatawadha kwaajili yao udhu wa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akamimina maji kwenye mikono yake kutoka katika bakuli, akaosha mikono yake mara tatu, kisha akaingiza mkono wake katika bakuli, akasukutua na akapandisha maji puani na akapenga mara tatu kwa kuchota mara tatu, kisha akaingiza mkono wake akaosha uso wake mara tatu, kisha akaingiza mkono wake katika bakuli akaiosha mara mbili mpaka katika viwiko viwili, kisha akaingiza mkono wake katika bakuli, akapaka maji kichwa chake, akaipeleka mikono yake mbele ya kichwa na akairudisha nyuma akafanya hivyo mara moja, kisha akaosha miguu yake). Na katika riwaya nyingine: (Alianza na mbele ya kichwa chake, akaenda nayo mpaka kisogoni kwake, kisha akairudisha mpaka sehemu alipoanzia). Na katika riwaya: (Alitujia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- tukamtolea maji katika bakuli la shaba).
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Kwasababu ya pupa ya wema waliotangulia -Mwenyezi Mungu awarehemu- juu ya kufuata mafundisho (sunna) walikuwa wakiuliza juu ya namna ya kazi za Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ili waige Sunna zake,na katika hadithi hii anaelezea Amru bin Yahya Al Maaziniy kutoka kwa baba yake:yakwamba yeye alimshuhudia baba yake mdogo Amru bin Hasan, akimuuliza Abdallah bin Zaidi mmoja kati ya maswahaba -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuhusu namna ya udhu wa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-; akataka Abdullah ambainishie kwa sura ya kivitendo; kwasababu hili ni jepesi kulielewa,na hutazamwa kwa undani zaidi na hukita zaidi katika nafsi,akaomba chombo cha maji,akaanza kwa kuosha viganja vyake; kwasababu viganja ndio hutumika kuoshea na kuchukulia maji, akainamisha chombo akaiosha mara tatu, kisha akaingiza mkono wake katika chombo, akachota humo machoto matatu akawa anasukutua kwa kila choto na anapandisha maji puani na kuyapenga,kisha akachota maji na akaosha uso wake mara tatu, kisha akachota choto akaosha mikono yake mpaka katika viwiko viwili mara mbili mbili, kisha akaingiza mikono yake katika maji akafuta kwa mikono yake miwili mbele ya kichwa chake mpaka akafika kisogoni kwake juu kidogo ya shingo, kisha akairudisha mpaka akafika nayo sehemu aliyoanzia, alifanya hivi, ili zipokee upako nywele za kichwa na anazirudisha nyuma ili akieneze kichwa juu yake na ndani yake,kisha akaosha miguu yake mpaka katika fundo mbili, na akabainisha Abdullah bin Zaidi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa hiki ni kitendo cha Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- pale alipowajia,wakamtolea maji katika bakuli la shaba;ili atawadhie Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- alibainisha hivyo Abdullah; ili athibitishe kuwa yeye alikuwa na uhakika juu ya jambo hilo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama