عن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه مرفوعًا: «ليس مِنْ نَفْسٍ تُقْتَلُ ظُلماً إِلاَّ كَان على ابنِ آدَمَ الأَوَّل كِفْلٌ مِن دمِهَا؛ لِأَنَّه كان أوَّل مَن سَنَّ القَتْلَ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdallah bin Mas'udi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-Hadithi Marfu'u: "Haitokei kuuliwa nafsi yoyote kwa dhulma isipokuwa hupata binadamu wa mwanzo fungu (la dhambi) kutoka katika damu hiyo, kwasababu yeye ndiye muanzilishi wa kwanza kuua".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Inasimulia hadithi hii sababu ya kubebeshwa mmoja kati ya binadamu damu zinazofuatia ambazo zinazomwagwa baada yake, Inasemekana kuwa ni Qaabil alimuua ndugu yake Haabil kwasababu ya kumuhusudu, wao ndio muuliwa na muuwaji wa mwanzo katika watoto wa adamu; anabeba Qaabil fungu la madhambi ya damu ambazo zinazomwagwa baada yake; kwasababu yeye ndiye aliyeanzilisha kuuwa; kwasababu kila atakayefanya baada yake anaiga kwake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama