عن عبد الله بن عمر رضي الله عنهما قال: كان النبي صلى الله عليه وسلم يزورُ قُبَاءَ راكبًا وماشيًا، فيُصَلِّي فيه ركعتين. وفي رواية: كان النبي صلى الله عليه وسلم يأتي مسجد قُبَاءَ كل سَبْتٍ راكبًا وماشيًا، وكان ابن عُمر يفعله.
[صحيح] - [الرواية الأولى: متفق عليها. الرواية الثانية: متفق عليها]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdallah bin Omar -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Amesema: Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akiitembelea msikiti wa Qubaa kwa kipando na kwa miguu, anaswali ndani yake rakaa mbili. Na katika riwaya nyingine: Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akienda msikiti wa Qubaa kila juma mosi akiwa katika kipando na kwa miguu, na alikuwa bin Omar akifanya hivyo.
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy na Muslim kwa riwaya zake

Ufafanuzi

Eneo la Qubaa ambapo umejengwa hapo msikiti wa kwanza katika uislamu ni kijiji kilichopo karibu na kituo cha Madina tokea pande za kusini mashariki ya mji wa Madina,akawa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- anautembelea msikiti wa Qubaa akiwa katika kipando na akiwa kwa miguu, na aliposema kila juma mosi: makusudio nikuwa alikuwa akitenga baadhi ya siku kwaajili ya ziara, na hekima ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake kuja Qubaa siku ya juma mosi katika kila wiki, ilikuwa ni ajili ya kuunga udugu na maanswari na kujua hali zao na hali ya yule aliyechelewa kuipata swala ya ijumaa pamoja naye,na hii ndio siri ya kuichagua ziara katika sikuya juma mosi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kireno
Kuonyesha Tarjama