+ -

عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم:
«مَلْعُون مَنْ أتَى امرأتَه في دُبُرِها».

[حسن] - [رواه أبو داود والنسائي في الكبرى وأحمد] - [سنن أبي داود: 2162]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema: Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-:
"Amelaaniwa mwenye kumuingilia mke wake kinyume na maumbile".

[Ni nzuri] - - [سنن أبي داود - 2162]

Ufafanuzi

Anamtahadharisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake mwanaume kumuingilia mkewe katika utupu wake wa nyuma; kuwa amelaaniwa na amefukuzwa kutoka katika rehema ya Mwenyezi Mungu, nalo ni dhambi katika madhambi makubwa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kikurdi Kireno Kiassam الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Uharamu wa kuwaingilia nyuma wanawake.
  2. Kustarehe na mke sehemu yoyote katika mwili wake isiyokuwa nyuma inafaa.
  3. Muislamu anamuingilia mwanamke katika tupu yake ya mbele kama alivyomuamrisha Mwenyezi Mungu; na ama kwa nyuma kuna kuharibu maumbile, na kupoteza kizazi, na kwenda kinyume na asili salama ya viumbe hai, na kuna madhara makubwa kati ya wanandoa.