+ -

عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رضي الله عنهما قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«لَا يَنْظُرُ اللهُ إِلَى رَجُلٍ أَتَى رَجُلًا أَوِ امْرَأَةً فِي دُبُرٍ».

[صحيح] - [رواه الترمذي والنسائي في الكبرى] - [السنن الكبرى للنسائي: 8952]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Bin Abbas -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake-:
"Hamtazami Mwenyezi Mungu mtu ambaye kamuingilia mwanaume au mwanamke katika tupu yake ya nyuma".

[Sahihi] - - [السنن الكبرى للنسائي - 8952]

Ufafanuzi

Amebainisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake ahadi kali ya adhabu kuwa Mwenyezi Mungu hatomtazama mtazamo wa huruma mwanaume aliyemuingilia mwanaume mwenzake katika utupu wake wa nyuma, au mwanamke katika utupu wake wa nyuma, nakuwa hilo ni dhambi kubwa katika madhambi makubwa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kikurdi Kireno Kiassam الأمهرية الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Mwanaume kumwendea mwanaume mwenzake (Ulawiti) ni katika madhambi makubwa.
  2. Kumwendea mwanamke katika tupu yake ya nyuma ni katika madhambi makubwa.
  3. "Hamtazami Mwenyezi Mungu" Yaani: Mtazamo wa huruma au upole, na si makusudio yake: Kutazama kwa ujumla; kwa sababu Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka hakuna chochote kinachofichikana kwake na hakitoweki machoni mwake chochote.
  4. Matendo haya ni katika machafu makubwa na ni hatari sana kwa binadamu; kwakuwa ndani yake kuna kwenda kinyume na maumbile salama ya kibinadamu, na kupungua kwa kizazi, na kuharibu maisha ya ndoa, na kupandikiza uadui na chuki, na kuingia katika maeneo machafu yenye kutia kinyaa.
Ziada