عن حمران مولى عثمان أنَّه رأى عثمان دعا بوَضُوء، فأفرَغ على يَدَيه مِن إنائه، فغَسَلهُما ثلاثَ مرَّات، ثمَّ أدخل يَمينَه في الوَضُوء، ثمَّ تَمضمَض واستَنشَق واستَنثَر، ثُمَّ غَسل وَجهه ثَلاثًا، ويديه إلى المرفقين ثلاثا، ثم مسح برأسه، ثمَّ غَسل كِلتا رجليه ثلاثًا، ثمَّ قال: رأيتُ النَّبِي صلى الله عليه وسلم يتوضَّأ نحو وُضوئي هذا، وقال: (من توضَّأ نحو وُضوئي هذا، ثمَّ صلَّى ركعتين، لا يحدِّث فِيهما نفسه غُفِر له ما تقدَّم من ذنبه).
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Humran maula othman, yakwamba yeye alimuona othman akiomba chombo cha udhu, akamimina mikononi mwake kutoka katika chombo chake, akaiosha mara tatu, kisha akaingiza mkono wake wa kulia katika chombo cha udhu, kisha akasukutua na akapandisha maji puani na akapenga, kisha kaosha uso wake mara tatu, na mikono yake mpaka katika viwiko viwili mara tatu, kisha akakifuta kichwa chake, kisha akaosha miguu yake yote miwili mara tatu, kisha akasema: Nilimuona Mtume rehema na Amani zimfikie akitawadha mfano wa udhu wangu huu, na akasema: "Yeyote atakayetawadha mfano wa udhu wangu huu, kisha akasali rakaa mbili, na asiizungumzishe ndani ya nafsi yake atasamehewa yaliyotangulia katika madhambi yake".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Imekusanya hadithi hii tukufu juu ya sifa kamili za udhu wa Mtume rehema na Amani zimfikie- Kwasababu othman kwa mafundisho yake mazuri na uzuri wa uelewa wake kawafundisha sifa ya udhu wa Mtume rehema na Amani zimfikie kwa njia ya kitaalamu, ili iweze kufahamika vizuri zaidi, kwani aliomba chombo chenye maji, na ili asiyachafue maji hakuanza kwa kutumbukiza vidole vyake ndani yake, bali alimimina katika mikono yake mara tatu mpaka ikawa misafi, baada ya hapo aliingiza mkono wake wa kulia katika chombo na akachukulia maji akasukutua na akapandisha puani na akapenga, kisha akaosha uso wake mara tatu, kisha akaosha mikono yake pamoja na viwiko vyake mara tatu, kisha akafuta kichwa chake chote mara moja, kisha akaosha miguu yake na fundo mbili mara tatu. Alipomaliza radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake katika zoezi hili na udhu ulio kamili, aliwaeleza kuwa yeye alimuona Mtume rehema na Amani zimfikie alitawadha mfano wa udhu huu, na akawaeleza Mtume rehema na Amani zimfikie kwamba yeyote atakaye tawadha mfano wa udhu wake, na akaswali rakaa mbili, kwa unyenyekevu na kuhudhurisha moyo wake mbele ya Mola wake aliyetakasika na kutukuka ndani ya hizo rakaa mbili, basi bila shaka kwa fadhila za Mwenyezi Mungu Mtukufu atamlipa kwa udhu huu uliokamilika, na kwa hii swala yenye utakasifu, kwa kumsamehe yaliyotangulia katika madhambi yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ubora wa kiongozi wa waumini othman radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, na pupa yake ya kusambaza elimu na sunna.
  2. Kufundisha kwa vitendo kwakuwa ndio inaeleweka zaidi na ina udhibiti mzuri.
  3. Ni sunna kuosha mikono miwili kabla ya kuiingiza katika chombo cha udhu, hata kama mtu hajaamka kutoka usingizini, na ikiwa mtu kaamka kutoka katika usingizi wa usiku basi ni wajibu kuiosha.
  4. Atakayefanya ibada kwaajili ya Mwenyezi Mungu, na akakusudia pamoja na hilo kuwafundisha watu, hilo halipunguzi chochote katika Ikhlasi yake (utakasifu wake wa nia).
  5. Inatakiwa mwalimu atumie njia yenye ukaribu zaidi katika uelewa na kuifanya elimu ikite vizuri kwa wanafunzi.
  6. Inatakiwa mwenye kuingia katika ibada azuie fikra zinazoambatana na shughuli za kidunia, na apambane na nafsi katika hilo, kwasababu mtu humuijia akiwa katika swala yake yale aliyonatamaanayo.
  7. Ni sunna kuanzia kulia katika udhu na katika kuchukua maji ya udhu kwaajili ya kuosha viungo.
  8. Sheria ya kufuata mpangilio kati ya kusukutua na kupandisha maji puani, na kupenga.
  9. kuosha uso mara tatu.
  10. Kufuta kichwa chote mara moja.
  11. Kuosha miguu miwili pamoja na fundo mbili mara tatu.
  12. Ulazima wa kufuata mpangilio katika hilo, kwasababu Mwenyezi Mungu ameamrisha kufuta kichwa na akakiingiza kati ya kuosha miguu miwili na viungo vingine, jambo linaloonyesha uwajibu wa kufuata mpangilio.
  13. Sifa hii ndio sifa ya udhu wa Mtume rehema na Amani zimfikie iliyokamilika.
  14. Kuwekwa sheria ya kuswali baada ya udhu.
  15. Sababu ya kutimia swala na ukamilifu wake, ni moyo kuhudhuria mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na tahadhari ya kutopokelewa swala kwa yule atakayepumbazika ndani yake kwa mambo ya kidunia, na zitakayejitokeza kwake fikra za kidunia naye akiwa katika swala akazifukuza, anatarajiwa kwake kupata malipo haya.
  16. Kuosha mikono miwili pamoja na viwiko viwili mara tatu.
  17. Thawabu na malipo yaliyoahidiwa hapo, yanaambatana na jumla ya mambo mawili, nayo ni kutia udhu kwa sifa iliyotajwa, na kuswali rakaa mbili kwa sifa iliyotajwa.
  18. Malipo ya udhu na kuswali rakaa mbili kwa unyenyekevu, ni kusamehewa na Mwenyezi Mungu yaliyotangulia katika madhambi.