عن أبي هريرة، قال: أتَى النبي صلى الله عليه وسلم رجُلٌ أعْمَى، فقال: يا رسول الله، إنه ليس لي قائد يَقُودُني إلى المسجد، فَسَأل رسول الله صلى الله عليه وسلم أن يُرَخِّص له فيصلِّي في بَيْتِه، فرَخَّص له، فلمَّا ولىَّ دَعَاه، فقال: «هل تسمع النِّداء بالصلاة؟» قال: نعم، قال: «فأجِب».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira, Amesema: Alimuijia Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake mtu kipofu, Akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hakika sina muongozaji wa kuniongoza njia kuja msikitini, akamuomba Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake amruhusu aswalie nyumbani kwake, akamruhusu, alipogeuka kuondoka akamuita, kisha akasema: "Je unasikia wito wa swala?" Akasema: Ndiyo, akasema: "basi itikia wito wa sala".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Alikuja mtu kipofu kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-, akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mtu kipofu sina wa kunisaidia na kunishika mkono mpaka msikitini, katika swala tano, akitaka amruhusu Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- kuacha jamaa, akamruhusu, alipogeuka kuondoka akamuita na akasema: Je unasikia adhana ya swala? Akasema: Ndiyo. Akasema: Basi muitike mnadi swala.