عن عثمان بن عفان رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «من توضَّأ فَأَحْسَن الوُضُوءَ، خَرَجَتْ خَطَايَاهُ مِنْ جَسَدِهِ حَتَّى تَخْرُج مِنْ تَحْتِ أَظْفَارِه».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Othmani bin A'ffani -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Atakayetawadha na akaufanya vizuri udhu, yatatoka madhambi yake mwilini mwake,mpaka yanatokea chini ya kucha yake".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Hadithi inaonyesha kuwa udhu ni katika ibada bora, na katika ubora wake ni ule uliokuja katika hadithi hii kuwa Atakayetawadha na akaufanya vizuri udhu, kiasi kwamba kazingatia sunna zake na adabu zake, utakuwa udhu wake huu ni sababu ya kutoka yale madhambi madogo madogo aliyoyachuma yanayohusiana na haki ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, mpaka yatoke makosa na madhambi haya katika sehemu nyembamba nayo ni ile iliyochini ya kucha, na kwaajili hii sasa inampasa mtu anuie kwa udhu wake kujiweka karibu na Mwenyezi Mungu Mtukufu, na avute hisia kuwa yeye anatekeleza amri ya Mwenyezi Mungu katika kauli yake: "Mtakaposimama kutaka kusali,basi osheni nyuso zenu" Al-Maidah: 6, Na avute hisia pia kuwa yeye anamfuata Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- katika udhu wake, Na ajihisi pia kuwa anataka malipo, nakuwa yeye analipwa juu ya amali hii ili aifanye kwa ufanisi na uzuri zaidi.