عن عثمان بن عفان رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «من توضَّأ فَأَحْسَن الوُضُوءَ، خَرَجَتْ خَطَايَاهُ مِنْ جَسَدِهِ حَتَّى تَخْرُج مِنْ تَحْتِ أَظْفَارِه».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Othmani bin A'ffani -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Atakayetawadha na akaufanya vizuri udhu, yatatoka madhambi yake mwilini mwake,mpaka yanatokea chini ya kucha yake".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Hadithi inaonyesha kuwa udhu ni katika ibada bora, na katika ubora wake ni ule uliokuja katika hadithi hii kuwa Atakayetawadha na akaufanya vizuri udhu, kiasi kwamba kazingatia sunna zake na adabu zake, utakuwa udhu wake huu ni sababu ya kutoka yale madhambi madogo madogo aliyoyachuma yanayohusiana na haki ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, mpaka yatoke makosa na madhambi haya katika sehemu nyembamba nayo ni ile iliyochini ya kucha, na kwaajili hii sasa inampasa mtu anuie kwa udhu wake kujiweka karibu na Mwenyezi Mungu Mtukufu, na avute hisia kuwa yeye anatekeleza amri ya Mwenyezi Mungu katika kauli yake: "Mtakaposimama kutaka kusali,basi osheni nyuso zenu" Al-Maidah: 6, Na avute hisia pia kuwa yeye anamfuata Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- katika udhu wake, Na ajihisi pia kuwa anataka malipo, nakuwa yeye analipwa juu ya amali hii ili aifanye kwa ufanisi na uzuri zaidi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuhimizwa juu ya kuzingatia kujifunza adabu za udhu na sharti zake, na kulifanyia kazi hilo.
  2. Kubainishwa fadhila za udhu, nakuwa ni kafara ya madhambi.
  3. Sharti la kutoka kwa makosa ni kuufanya vizuri udhu na kuuleta kama alivyoweka wazi Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake.
  4. Kuhimizwa juu ya kuzingatia kujifunza sharti za udhu na sunna zake na adabu zake, na kulifanyia kazi hilo.