عن عقبة بن عامر رضي الله عنه مرفوعاً: «إن أحَقَّ الشُّروط أن تُوفُوا به: ما استحللتم به الفروج».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Uqbah bin Aamir -Radhi za Allah ziwe juu yake- akisimulia kutoka kwa Mtume: " Hakika masharti yenye haki zaidi ya nyinyi kuyatekeleza ni yale mliyohalalisha kwayo nyuchi".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Kila mmoja katika wanandoa ana makusudio na malengo ya kudumu katika mkataba wa ndoa, hivyo akaweka sharti kwa mwenzie ili ashikamane nazo na akataka zitekelezwe, na zinaitwa kuwa ni sharti katika ndoa, nazo ni zile zinazozidi katika sharti za ndoa ambazo ndoa haikubaliki ispokuwa kwa sharti hizo. Na umekuja msisitizo juu ya kuzitekeleza; kwasababu sharti katika ndoa zina heshima kubwa na kuzitimiza na kuzizingatia ni lazima; kwa kuwa kwake zimestahiki kuhalalisha na kustarehe na tupu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ulazima wa kutekeleza masharti ambayo ameshikamana nayo mmoja kati ya wanandoa wawili kwa mwenzie, na hayo ni kama kuweka sharti la ziada ya mahari au makazi katika sehemu maalumu kutoka upande wa mwanamke, na kama kuweka sharti la bikra na nasaba, toka upande wa mume.
  2. Kuna dhibitiwa kutokuenea kwa hukumu ya hadithi kwa ulazima wa kutekeleza masharti, ni sawa na mfano wa hadithi (Si halali kwa mwanamke kuomba kupewa talaka dada yake).
  3. Nikuwa kutekelezwa kwa masharti ya ndoa kumetiliwa mkazo zaidi kuliko kutekelezwa kwa masharti mengineyo, kwasababu kunaambatana na kuhalalisha tupu.
  4. Nikuwa yanayotakiwa kwa kila mmoja kati ya wanandoa wawili juu ya mwenzie ni kama matumizi na kustarehe na malazi kwa mwanamke, pia kama kustarehe kwa mume haya hayana kiwango, bali yanarudishwa katika mazoea ya watu.
  5. Sharti katika ndoa zina sehemu mbili: sahihi nazo ni: (a): zile zisizoenda kinyume na lengo la makubaliano, na awe mtoa sharti ana lengo sahihi. (b): Za batili: nazo ni zile zinazokwenda kinyume na makubaliano. Na kipimo katika sharti hizi na mfano wake, ni kauli yake Rehema na Amani ziwe juu yake- "Waislamu wanatakiwa kufungamana na sharti zao, ispokuwa sharti lililoharamisha halali au kuhalalisha haramu" na hakuna tofauti kati kutokea sharti kabla au wakati wa kufunga ndoa.