عن قيس بن عاصم رضي الله عنه قال:
أتيتُ النبيَّ صلى الله عليه وسلم أُريدُ الإسلامَ، فأَمَرَني أن أغتَسِلَ بماءٍ وسِدرٍ.

[صحيح] - [رواه أبو داود والترمذي والنسائي]
المزيــد ...

Kutoka kwa Kaisi bin Aswim -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema:
Nilimwendea Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- nikitaka kuwa muislamu, akaniamrisha nioge kwa maji na mkunazi.

Sahihi - Imepokelewa na Abuu Daud

Ufafanuzi

Alikuja Kaisi bin Aswim kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akitaka kusilimu, Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akamuamrisha aoge kwa maji na mti wa mkunazi; kwakuwa majani yake hutumika katika usafi; na kwakuwa yana harufu nzuri.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Sheria ya kafiri kuoga anapoingia katika Uislamu.
  2. Thamani ya Uislamu na kutilia kwake umuhimu mwili na roho vyote kwa pamoja.
  3. Maji kuchanganyika na vitu safi haviyatoa katika twahara yake.
  4. Visimama badala ya mkunazi vifaa vya usafi vya kisasa, kama sabuni na mfano wake.