عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «من كان يؤمن بالله واليوم الآخر فليقل خيرًا أو ليصْمُت، ومن كان يؤمن بالله واليوم الآخر فليُكْرِم جارَه، ومن كان يؤمن بالله واليوم الآخر فليكرم ضَيْفَه».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Yeyote mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na aseme la kheri au anyamaze, Na Yeyote mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na amkirimu jirani yake, Na Yeyote mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na amkirimu mgeni wake".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Amesimulia Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Misingi ya kijamii ya kiujumla, Akasema: "Yeyote mwenye kumuamini" Hii ni sentensi ya sharti, jibu lake: "Basi na aseme kweli au anyamaze", Na makusudio ya sentensi hii ni kuhimiza na kuchochea juu ya kusema mambo ya kheri au kunyamaza, kana kwamba anasema: ikiwa kweli unamuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi sema la kheri au nyamaza. "Basi na aseme la kheri au anyamaze" kama mtu kusema kauli ambayo si ya kheri katika nafsi yake lakini ni kwaajili ya kuwafurahisha wale aliokaa nao, kwani hii ni kheri kwa yale yanayoambatana nayo kama kuwaliwaza na kuondoa upweke na kupatikana mapenzi. "Au anyamaze" Yaani akae kimya. "Na mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na amkirimu jirani yake" Yaani jirani katika nyumba, na inavyoonyesha nikuwa inakusanya hata jirani yake katika biashara kama jirani katika duka mfano, japo kwa ujirani wa kwanza ndiyo bora zaidi, yaani ujirani katika nyumba, na kila anavyozidi kuwa karibu nawewe jirani ndivyo haki yake inavyozidi kuwa kubwa. Na akauita Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kuwa ni ukarimu akasema: "Basi na amkirimu jirani yake" na wala hakusema na ampe dirham (au shilingi) au sadaka au nguo au mfano wake, na kila kitu kinachokuja kwa ujumla katika sheria bila ufafanuzi basi hicho kinarudi katika mazoea ya watu. Hivyo ukarimu haujaainishwa, bali kila ambacho watu wanakichukulia kuwa ni ukarimu, na jirani yako mwenye hali ya chini huenda akatosheka na kitu kidogo katika ukarimu wako, na jirani yako mwenye cheo anahitaji zaidi ya hapo. Na jirani: Je ni yule aliye na mafungamano au mnayeshirikiana naye sokoni au ni yule mnayetazamana au ni yupi? Hili pia linarudi katika mazoea ya watu. Na ama katika kauli yake Rehema na Amani ziwe juu yake: "Na yeyote mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi na amkirimu mgeni wake" Mgeni ni yule aliyeshuka kwako, kama mtu msafiri aliyeshuka kwako, huyu ni mgeni ni wajibu kumkirimu kwa kila kinachohesabika kuwa ni ukarimu. Wamesema baadhi ya wa wanachuoni- Mwenyezi Mungu awarehemu- Hakika ni wajibu ugeni katika vijiji au miji midogo, ama katika majiji na miji mikubwa si wajibu; kwasababu miji hii ndani yake kuna migahawa na hoteli anaweza kwenda huko, lakini miji midogo anahitaji mtu sehemu ya kujihifadhi. Lakini uwazi wa hadithi nikuwa inajumuisha yote "Basi na amkirimu mgeni wake".

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Tahadhari kutokana na maafa ya ulimi, nakuwa ni lazima kwa mtu ayatafakari yale anayotaka kuyazungumza.
  2. Ulazima wa kunyamaza ispokuwa katika mambo ya kheri.
  3. Maana ya haki ya jirani, na kuhimizwa juu ya kuhifadhi ujirani wake na kumkirimu.
  4. Amri ya kumkirimu mgeni, nayo ni katika adabu za uislamu na ni tabia ya Manabii.
  5. Dini ya uislamu ni dini ya mapenzi na ukaribu na kujuana tofauti na dini zingine.
  6. Kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho ndiyo msingi wa kila kheri, na ni msukumo wa kuchunga sheria na hofu na matumaini kwa Mwenyezi Mungu, na inaambatana na mwanzo -tulikotoka- na marejeo- yetu baada ya hapa-, na ni msukumo mkubwa katika kutekeleza sheria.
  7. Maneno kuna ya kheri na ya shari, na yasiyokuwa ya kheri wala ya shari.
  8. Hakika mambo haya ni katika sehemu ya imani na ni katika adabu tukufu.
  9. Nikuwa matendo yanaingia katika imani.
  10. Nikuwa imani inaongezeka na kupungua.