عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم:
«مَنْ كَذَبَ عَلَيَّ مُتَعَمِّدًا فَلْيَتَبَوَّأْ مَقْعَدَهُ مِنَ النَّارِ».

[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Imepolelewa Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: amesema: Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-:
"Yeyote atakayenisingizia mimi uongo kwa makusudi basi ajiandalie makazi yake kuwa ni motoni".

Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa atakayemsemea uongo kwa makusudi kwa kumnasibishia kauli au kitendo kwa uongo, basi atambue kuwa Akhera atakua na makazi motoni; ndio malipo yake kwa kumsingizia kwake uongo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Kichina Kifursi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kimalayo Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kumsemea uongo Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kwa makusudi kabisa ni sababu ya kuingia motoni.
  2. Kumsemea uongo Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- si sawa na kuwasemea uongo watu wengine, kwa kuwa hilo linaambatana na madhara makubwa katika dini na dunia.
  3. Hii ni tahadhari ya kusambaza hadithi kabla ya kuthibitisha usahihi wake kuwa ni kweli zimenasibishwa kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- au la!.