عن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما : أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «بلغوا عني ولو آية، وحدثوا عن بني إسرائيل ولا حرج، ومن كذب علي متعمدا فَلْيَتَبَوَّأْ مقعده من النار».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillahi bin Amri bin Aaswi- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao-: Yakwamba Mtume Rehema na Amani zimfikie Amesema: "Fikisheni toka kwangu walau Aya moja, na simulieni kuhusu wana wa Israeli wala hakuna tabu, na atakayenizulia uongo juu yangu kwa makusudi basi ajiandalie makazi yake motoni".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Maana ya hadithi nikuwa wahamishieni watu elimu iliyorithiwa toka kwangu kutoka katika kitabu (Qur'ani) na Sunna, hata kama kitakuwa kile mnachokifikisha ni kichache kama Aya moja ya Qur'ani, kwa sharti awe na uhakika na kile anachokifikisha, na Amri ya kufikisha iko katika ulazima linapolazimu hilo juu ya mtu, na lisipolazimu hilo juu yake, kama kuwepo katika mji walinganizi kwa Mwenyezi Mungu wanaosimamia kuwafundisha watu na kuwaelekeza mambo yao, hapo hakuna uwajibu kwake wa kufikisha, bali inapendeza kwake (ni sunna kwake) kufanya hivyo, na hakuna tatizo na wala hakuna dhambi kwenu mkizungumza kuhusu wana wa Israeli kwa yale yaliyotokea kwao katika matukio ya kweli, kama kushuka moto kutoka mbinguni kwaajili ya kula sadaka, na kama simulizi za kujiuwa katika toba yao kwa kuabudu ndama, au kuvifafanua visa vilivyotajwa katika Qur'ani ambavyo ndani yake vina mazingatio na mawaidha, na atakayenizulia juu yangu uongo basi ajiandalie kwaajili ya nafsi yake makazi motoni, na hilo, ni kwasababu uongo juu ya Mtume Rehema na Amani zimfikie si kama kuwazulia watu wengine, kumzulia uongo Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani zimfikie ni kumzulia Mwenyezi Mungu Mtukufu, kisha ni kuizulia uongo sheria; kwasababu anayoyaeleza Mtume rehema na Amani zimfikie nikatika wahyi ambao ni sheria ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, ndio maana adhabu yake ikawa kali.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ulazima wa kufikisha sheria ya Mwenyezi Mungu, nakuwa mtu atimize yale aliyoyahifadhi na akayaelewa hata kama ni kidogo.
  2. Ulazima wa kutafuta elimu, ili mtu aweze kuifikisha sheria ya Mwenyezi Mungu, nayo ni katika faradhi ya kujitosheleza ambayo wakiisimamia baadhi ya waislamu unaondoka ulazima kwa waliobakia, na asiposimamia yeyote wote wanapata madhambi.
  3. Ruhusa ya kuzungumza yale yaliyojiri kwa wana wa Israeli; kwaajili ya kuchukua mazingatio na mawaidha, kwa sharti yasiwe mazungumzo katika yale yaliyothibiti uongo wake, na atafute yaliyothibiti na yaliyo karibu na sheria ya uislamu.
  4. Kuharamishwa uongo juu ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- nao ni katika madhambi makubwa.
  5. Kuhimizwa juu ya ukweli katika maneno na kuchukua tahadhari katika mazungumzo, ili asije kuangukia katika uongo, na hasa hasa katika sheria ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Na hili linahitaji elimu sahihi na ya ndani sana.