عن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما : أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «بلغوا عني ولو آية، وحدثوا عن بني إسرائيل ولا حرج، ومن كذب علي متعمدا فَلْيَتَبَوَّأْ مقعده من النار».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillahi bin Amri bin Aaswi- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao-: Yakwamba Mtume Rehema na Amani zimfikie Amesema: "Fikisheni toka kwangu walau Aya moja, na simulieni kuhusu wana wa Israeli wala hakuna tabu, na atakayenizulia uongo juu yangu kwa makusudi basi ajiandalie makazi yake motoni".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Maana ya hadithi nikuwa wahamishieni watu elimu iliyorithiwa toka kwangu kutoka katika kitabu (Qur'ani) na Sunna, hata kama kitakuwa kile mnachokifikisha ni kichache kama Aya moja ya Qur'ani, kwa sharti awe na uhakika na kile anachokifikisha, na Amri ya kufikisha iko katika ulazima linapolazimu hilo juu ya mtu, na lisipolazimu hilo juu yake, kama kuwepo katika mji walinganizi kwa Mwenyezi Mungu wanaosimamia kuwafundisha watu na kuwaelekeza mambo yao, hapo hakuna uwajibu kwake wa kufikisha, bali inapendeza kwake (ni sunna kwake) kufanya hivyo, na hakuna tatizo na wala hakuna dhambi kwenu mkizungumza kuhusu wana wa Israeli kwa yale yaliyotokea kwao katika matukio ya kweli, kama kushuka moto kutoka mbinguni kwaajili ya kula sadaka, na kama simulizi za kujiuwa katika toba yao kwa kuabudu ndama, au kuvifafanua visa vilivyotajwa katika Qur'ani ambavyo ndani yake vina mazingatio na mawaidha, na atakayenizulia juu yangu uongo basi ajiandalie kwaajili ya nafsi yake makazi motoni, na hilo, ni kwasababu uongo juu ya Mtume Rehema na Amani zimfikie si kama kuwazulia watu wengine, kumzulia uongo Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani zimfikie ni kumzulia Mwenyezi Mungu Mtukufu, kisha ni kuizulia uongo sheria; kwasababu anayoyaeleza Mtume rehema na Amani zimfikie nikatika wahyi ambao ni sheria ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, ndio maana adhabu yake ikawa kali.