عن أبي ذر الغفاري رضي الله عنه مرفوعاً: «لا تَحْقِرَنَّ من المعروف شيئا، ولو أن تَلْقَى أخاك بوجه طَلْق».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Dhari Al-Ghifariy- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Usidharau kabisa katika wema kitu chochote, hata kama ni kukutana na ndugu yako kwa uso mkunjufu".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Hadithi inaonyesha juu ya kupendeza kuwa na uso mkunjufu wakati wa kukutana, nakuwa hili ni katika wema ambao inampasa muislamu aupupie na wala asiudharau, kwakuwa ndani yake kuna kumliwaza ndugu muislamu na kuingiza furaha kwake.