عن أبي ذر رضي الله عنه قال: قال لي النبي صلى الله عليه وسلم:
«لَا تَحْقِرَنَّ مِنَ الْمَعْرُوفِ شَيْئًا، وَلَوْ أَنْ تَلْقَى أَخَاكَ بِوَجْهٍ طَلْقٍ».

[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 2626]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Dhari -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Alisema kuniambia mimi Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-:
"Kamwe!, Usidharau chochote katika wema, hata kama ni kukutana na ndugu ukiwa na uso mkunjufu".

[Sahihi] - [Imepokelewa Imamu Muslim] - [Swahiih Muslim - 2626]

Ufafanuzi

Amehimiza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- juu ya kutenda wema, na mtu asiudharau hata kama utakuwa kidogo, na miongoni mwake ni ukunjufu wa uso kwa kutabasamu wakati wa kukutana, ni lazima kwa muislamu alipupie hilo; kwa sababu hujenga kuwa na ukaribu na ndugu yako muislamu na huingiza furaha kwake.

Katika Faida za Hadithi

  1. Fadhila za kupendana kati ya waumini, na kutabasamu na bashasha wakati wa kukutana.
  2. Ukamilifu wa sheria hii na kugusa kwake kila sekta, nakuwa imekuja na mambo yote ambayo yana masilahi kwa waislamu na kuunganisha umoja wao.
  3. Himizo la kutenda wema hata kama ni kidogo.
  4. Inapendeza kuingiza furaha kwa waislamu; kwani ndani yake kuna kuleta ukaribu baina yao.
Kuonyesha Tarjama
Lugha: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Ziada (67)