عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «ليس الشديد بالصُّرَعة، إنما الشديد الذي يملك نفسه عند الغضب».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Hadithi Marfu'u: "Hawi mtu mkali kwa miereka, hakika mkali ni yule anayemiliki nafsi yake wakati wa hasira".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Nguvu za kiuhalisia si hizi nguvu za viungo vya mwili, na wala mkali mwenye nguvu si yule anayewapiga miereka wengine siku zote, bali mwenye nguvu na mkali ni yule aliyepambana na nafsi yake na akaitenza nguvu pale ambapo inapozidiwa na hasira; kwasababu hili linaonyesha juu ya nguvu yake ya kuweza kujimiliki na kumzidia kwake shetani.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ubora wa upole, Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na pindi wanapokasirika wao husamehe".
  2. Kupambana na nafsi wakati wa hasira ni kugumu mno kuliko kupambana na adui.
  3. Uislamu kubadilisha maana ya nguvu ya zama za ujinga kuwa ni tabia njema, kunajenga utu wa muislamu wa kipekee; Hivyo mtu mwenye nguvu kuliko wote ni yule mwenye kumiliki nguvu ya nafsi yake na akaikatisha matamanio yake.
  4. Ulazima wa kujiweka mbali na hasira; kwasababu ya yale yaliyomo miongoni mwa madhara kwa mwili na nafsi na jamii kwa ujumla.
  5. Hasira ni sifa ya kibinadamu, huondoka kwa mambo mengi miongoni mwake ni kuimiliki nafsi.