عن جرير بن عبد الله رضي الله عنه مرفوعاً: «مَنْ لا يَرْحَمِ النَّاسَ لا يَرْحَمْهُ اللهُ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Jariri bin Abdillah Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Asiyewahurumia watu hatomuhurumia Mwenyezi Mungu".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Asiyewahurumia watu Mwenyezi Mungu Mtukufu hamuhurumii, na makusudio ya watu: watu ambao wanastahiki huruma na wanaostahiki hifadhi na mfano wao, na ama makafiri wanaotupiga vita hao hawahurumiwi, bali wanauwawa kwasababu Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema katika kumsifu Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- na maswahaba zake (Ni wakali kwa makafiri wanahurumiana wao kwa wao) Suratul-Fat-hi: 29.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuwataja watu maalumu bila kutajwa viumbe vingine ni kuwatilia umuhimu; na kama si hivyo basi huruma inatakiwa kwa viumbe wote.
  2. Huruma ni tabia tukufu, umechunga uislamu juu ya kuitukuza kwake katika nafsi ya mtu.
  3. Kuhurumiana kati ya watu ni sababu ya kuhurumiwa na Mwenyezi Mungu.
  4. Kuthibitisha huruma ya Mwenyezi Mungu nayo ni sifa halisia ya kwake Aliyetakasika na kutukuka tena kwa maana yake inayoonekana na kwa namna inayonasibiana na Utukufu wake.