عَنْ هِشَامِ بْنِ حَكِيمِ بْنِ حِزَامٍ رَضيَ اللهُ عنهما أَنَّهُ مَرَّ عَلَى أُنَاسٍ مِنَ الْأَنْبَاطِ بِالشَّامِ، قَدْ أُقِيمُوا فِي الشَّمْسِ، فَقَالَ: مَا شَأْنُهُمْ؟ قَالُوا: حُبِسُوا فِي الْجِزْيَةِ، فَقَالَ هِشَامٌ: أَشْهَدُ لَسَمِعْتُ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ:
«إِنَّ اللهَ يُعَذِّبُ الَّذِينَ يُعَذِّبُونَ النَّاسَ فِي الدُّنْيَا».
[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 2613]
المزيــد ...
Kutoka kwa Hisham bin Hakim bin Hizam radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake yeye na baba yake, ya kwamba yeye alipita kwa watu miongoni mwa Anbat huko Sham, wakiwa wamesimamishwa juani, akasema: Wamekuwaje? Wakasema: Wamefungwa kwa sababu ya jizia (kodi), akasema Hisham: Ninashuhudia kuwa nilimsikia Mtume rehema na amani ziwe juu yake akisema:
"Hakika Mwenyezi Mungu huwaadhibu wale wanaowaadhibu watu duniani"
[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 2613]
Alipita Hisham bin Hakim bin Hizam radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao, kwa wakulima wasiokuwa Waarabu huko Sham, wakiwa wamesimamishwa chini ya joto la Jua, akauliza kuhusu jambo lililowapata? Akaambiwa kuwa wamefanywa hivyo kwa sababu ya kutolipa Jizia (kodi) hali yakuwa wanauwezo wa kulipa. Amesema Hisham radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: Ninashuhudia kuwa hakika nilimsikia Mtume rehema na amani ziwe juu yake akisema: Hakika Mwenyezi Mungu huwaadhibu wale wanaowaadhibu watu duniani kwa dhuluma pasina haki.