عن أنس بن مالك رضي الله عنه مرفوعاً: «يَسِّرُوا وَلاَ تُعَسِّرُوا، وَبَشِّرُوا وَلاَ تُنَفِّرُوا».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Anas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Fanyeni wepesi na wala msifanye uzito, na toeni habari njema na wala msiwakimbize watu".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akipenda kupunguza na kufawanyia wepesi watu, hajawahi katu, kupewa hiyari na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kati ya mambo mawili ispokuwa alikuwa anachagua jepesi zaidi kati ya hayo mawili, madamu halijawa haramu jambo hilo, Fanyeni wepesi na wala msifanye uzito, Yaani: katika hali zote, na kauli yake: Na toeni habari njema na wala msifukuze watu: bishara ni kutoa habari ya kheri, kinyume cha kufukuza, na katika kufukuza ni kutoa habari mbaya.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Wajibu kwa muumini awavutie watu kwa Mwenyezi Mungu na awahamasishe katika kheri.
  2. Ni lazima kwa mwenye kuwalingania watu kwa Mwenyezi Mungu atazame kwa hekima namna ya kufikisha ujumbe wa uislamu kwa watu.
  3. Kutoa habari njema huleta furaha na utulivu na kumuelekea mlinganiaji na yale anayoyafikisha kwa watu.
  4. Kutia uzito kunasababisha kuwafukuza na kupuuza na kutia wasi wasi katika maneno ya mlinganiaji.
  5. Upana wa rehema za Mwenyezi Mungu kwa waja wake nakuwa yeye ameridhia kwao dini tukufu na sheria nyepesi.