عن أنس بن مالك رضي الله عنه مرفوعاً: «يَسِّرُوا وَلاَ تُعَسِّرُوا، وَبَشِّرُوا وَلاَ تُنَفِّرُوا».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Anas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Fanyeni wepesi na wala msifanye uzito, na toeni habari njema na wala msiwakimbize watu".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akipenda kupunguza na kufawanyia wepesi watu, hajawahi katu, kupewa hiyari na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kati ya mambo mawili ispokuwa alikuwa anachagua jepesi zaidi kati ya hayo mawili, madamu halijawa haramu jambo hilo, Fanyeni wepesi na wala msifanye uzito, Yaani: katika hali zote, na kauli yake: Na toeni habari njema na wala msifukuze watu: bishara ni kutoa habari ya kheri, kinyume cha kufukuza, na katika kufukuza ni kutoa habari mbaya.