+ -

عَنْ جَرِيرٍ رضي الله عنه عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:
«مَنْ يُحْرَمِ الرِّفْقَ يُحْرَمِ الْخَيْرَ».

[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 2592]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Othman -radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- amesema:
"Mwenye kunyimwa upole basi kanyimwa kheri yote"

[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 2592]

Ufafanuzi

Anatueleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa mwenye kunyimwa upole akawa hakuafikishwa katika mambo ya dini na dunia, na katika mambo yake mwenyewe, na yale anayoyafanya na wengine, basi atakuwa kanyimwa kheri yote.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Thai Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية النيبالية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Fadhila za upole na himizo la kujipamba na tabia hiyo, na kemeo la ukali.
  2. Upole hunyoosha kheri za Dunia na Akhera na hupanua mlango wa baraka, lakini ukali ni kinyume chake.
  3. Upole ni taji ambalo hutokana na tabia njema na amani, na jeuri hutokana na hasira na ufidhuli, ndio maana aliusifia sana upole Mtume rehema na amani ziwe juu yake, na akapitiliza katika kusifu.
  4. Alisema Sufian Al-Thauri Mwenyezi Mungu amrehemu, akiwaambia jamaa zake: Je, mnajua upole ni nini? Ni kuweka mambo mahali pake panapofaa, na ukali mahali pake panapofaa, na upole mahali pake panapofaa, upanga mahali pake panapofaa, na mjeledi mahali pake.