عن حذيفة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «لا يدخل الجنة قَتَّات».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Hudhaifa- Radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume- Rehma na amani ziwe juu yake- amesema: "Haingii peponi mfitinishaji".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake ahadi kali ya adhabu juu ya mwenye kufanya ufitinishaji- kuhamisha maneno kati ya watu kwa lengo la kuharibu-, nayo nikuwa hatoingia peponi mwanzoni, bali atatanguliwa na adhabu kwa kadiri ya dhambi lake, na mfitinishaji ni msengenyaji, na kitendo chake ni katika madhambi makubwa; kwa mujibu wa hadithi hii.

Kufanya Tarjama: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibaghali Kichina Kifursi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese German Kijapani
Kuonyesha Tarjama

Faida nyingi

  1. Usengenyaji ni katika madhambi makubwa; kwa yale yanayopatikana ndani yake katika athari mbaya, na mwisho mbaya.
  2. Nikuwa sheria hii imejengwa juu ya yote ambayo ndani yake yanaleta huruma kati ya watu.