عن سعد بن أبي وقاص –رضي الله عنه- مرفوعاً: "إنَّ اللهَ يُحبُّ العَبدَ التقيَّ الغنيَّ الخفيَّ".
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Sa'di bin Abii Waqas Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake hadithi Marfu'u: "Hakika Mwenyezi Mungu anampenda mja mchamungu mwenye kutosheka mwenye kujificha".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Amebainisha Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake sifa za mtu ambaye Mwenyezi Mungu Mtukufu anampenda akasema: "Hakika Mwenyezi Mungu anampenda mja mchamungu mwenye kutosheka mwenye kujificha" Mchamungu: Ni anayemuogopa Mwenyezi Mungu Mtukufu akatekeleza amri zake na akaepuka makatazo yake, akatekeleza wajibu na akayaepuka maharamisho, naye pamoja na hilo akamsifia kuwa ni mwenye kutosheka, ametosheka mwenyewe na kuwahitajia watu, ni mwenye kutoshelezwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu na yale yasiyokuwa yeye, hawaombi watu chochote na wala hajiingizi kwa watu kwa kujidhalilisha, bali yeye ametosheka na watu mwenye kutoshelezwa na Mola wake, hageuki kwa mwingine, naye ni mwenye kujificha hajidhihirishi na wala hashughuliki na kuonekana kwa watu au kunyooshewa vidole au watu kumzungumza.