عن سعد بن أبي وقاص –رضي الله عنه- مرفوعاً: "إنَّ اللهَ يُحبُّ العَبدَ التقيَّ الغنيَّ الخفيَّ".
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Sa'di bin Abii Waqas Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake hadithi Marfu'u: "Hakika Mwenyezi Mungu anampenda mja mchamungu mwenye kutosheka mwenye kujificha".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Amebainisha Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake sifa za mtu ambaye Mwenyezi Mungu Mtukufu anampenda akasema: "Hakika Mwenyezi Mungu anampenda mja mchamungu mwenye kutosheka mwenye kujificha" Mchamungu: Ni anayemuogopa Mwenyezi Mungu Mtukufu akatekeleza amri zake na akaepuka makatazo yake, akatekeleza wajibu na akayaepuka maharamisho, naye pamoja na hilo akamsifia kuwa ni mwenye kutosheka, ametosheka mwenyewe na kuwahitajia watu, ni mwenye kutoshelezwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu na yale yasiyokuwa yeye, hawaombi watu chochote na wala hajiingizi kwa watu kwa kujidhalilisha, bali yeye ametosheka na watu mwenye kutoshelezwa na Mola wake, hageuki kwa mwingine, naye ni mwenye kujificha hajidhihirishi na wala hashughuliki na kuonekana kwa watu au kunyooshewa vidole au watu kumzungumza.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ubora wa kujitenga na watu pamoja na kudumu na utiifu wa Mwenyezi Mungu pale inapohofiwa kuwepo fitina na watu kuharibika.
  2. Kubainishwa sifa zinazopelekea mapenzi ya Mwenyezi Mungu kwa waja wake, nayo ni uchamungu na unyenyekevu na kuridhika na yale aliyoyagawa Mwenyezi Mungu.
  3. Kuthibitisha sifa ya mapenzi kwa Mwenyezi Mungu- nayo ni kwa namna inayoendana naye- nakuwa yeye anampenda mja mtiifu.