عن أبي سعيد الخدري –رضي الله عنه- قال: خرج معاوية رضي الله عنه على حَلْقَةٍ في المسجد، فقال: ما أَجْلَسَكم؟ قالوا: جلسنا نذكر الله، قال: آلله ما أجْلَسَكُم إلا ذاك؟ قالوا: ما أجلسنا إلا ذاك، قال: أما إنّي لم استَحْلِفْكُم تُهْمَةً لكم، وما كان أحد بمنزلتي من رسول الله صلى الله عليه وسلم أقَلَّ عنه حديثاً مِنِّي: إنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم خَرَجَ على حَلْقَةٍ من أصحابه فقال: «ما أَجْلَسَكم؟» قالوا: جلسنا نذكر الله ونَحْمَدُهُ على ما هَدَانا للإسلام؛ ومَنَّ بِهِ علينا، قال: «آلله ما أجْلَسَكُم إلا ذاك؟» قالوا: والله ما أجلسنا إلا ذاك، قال: «أما إنّي لم أستحلفكم تُهْمَةً لكم، ولكنه أتاني جبريل فأخبرني أن الله يُبَاهِي بكم الملائكة».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu saidi Al-khudriy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Alitoka Muawiya- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- akakuta duara msikitini, akasema: Nini kimekukalisheni? wakasema: tumekaa tunamtaja Mwenyezi Mungu, akasema: Nawaapiza kwa Mwenyezi Mungu, hakika hakuna lililokukalisheni isipokuwa hilo? Wakasema: Hakuna lililotukalisha isipokuwa hilo, Akasema: Ama hakika mimi sikukuapizeni kwasababu ya kuwatuhumu, na hakuna yeyote mwenye mazungumzo kidogo kuliko mimi kutoka kwa Mtume, kutokana na nafasi yangu kwa Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake-: Hakika Mjumbe wa Mwenyezi Mungu alitoka akakuta duara la maswahaba zake akasema: "Nini kimekukalisheni?" Wakasema: Tumekaa tunamtaja Mwenyezi Mungu na tunamuhimidi kwa kule kutuongoza katika uislamu; na akauneemesha juu yetu; Akasema: "Nakuapizeni kwa Mwenyezi Mungu, je hakuna kilichokukalisheni isipokuwa hicho?" wakasema: Tunamuapa Mwenyezi Mungu hakuna kilichotukalisha isipokuwa hicho, Akasema: "Ama hakika mimi sikukuapizeni kwasababu ya kuwatuhumu, lakini uhakika nikuwa amenijia mimi Jibril akanieleza kuwa hakika Mwenyezi Mungu anajifaharisha kupitia nyinyi kwa Malaika".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Hadithi hii ni katika hadithi ambazo zinaonyesha ubora wa kukusanyika katika kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu, nayo ni hii aliyoipokea Abuu Saidi Al-Khudriy kutoka kwa Mua'wiya- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- yakwamba yeye alitoka akakuta duara la watu msikitini akawauliza wamekusanyika kwaajili ya jambo gani?, Wakasema: Tunamtaja Mwenyezi Mungu, Akawaapiza -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa wao hawakukusudia kwa kukaa kwao na kukusanyika kwao isipokuwa ni kumtaja Mwenyezi Mungu, wakamuapia, Kisha akasema kuwaambia: Hakika mimi sikuwaapizeni kwasababu ya kuwatuhumu nakuwa na shaka na ukweli wenu, lakini mimi nilimuona Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- alitoka kwa watu fulani na akataja mfano wa hayo, na akawaeleza kuwa hakika Mwenyezi Mungu -Aliyetakasika na Kutukuka- anajifaharisha kupitia wao kwa Malaika, Anasema kwa mfano: Tazameni waja wangu wamekusanyika kwaajili ya kunitaja, na mfano wake katika mambo ambayo ndani yake kuna kujifaharisha, Lakini kukusanyika huku si kwamba wajikusanye katika dhikri- kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu- kwa sauti moja, lakini wanataja jambo lolote linalowakumbusha kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kama mawaidha na ukumbusho, au wakakumbuka neema za Mwenyezi Mungu juu yao kwa kule kuwaneemesha juu yao kwa neema ya Uislamu na afya ya mwili na amani, na mfano wa hayo, kwani kukumbuka neema za Mwenyezi Mungu Mtukufu ni katika kumtaja Mwenyezi Mungu, Na kwa hili inakuwa ni ushahidi juu ya ubora wa watu kukaa ili wakumbushane neema za Mwenyezi Mungu juu yao.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo الدرية
Kuonyesha Tarjama