عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «ليس شيءٌ أكرمَ على الله من الدعاء».
[حسن] - [رواه الترمذي وابن ماجه وأحمد]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakuna kitu kitukufu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko dua".
Ni nzuri - Imepokelewa na Ibnu Maajah
(Hakuna kitu kitukufu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko dua) kwakuwa ni ibada, na ibada ni ile ambayo amewaumba Mwenyezi Mungu Mtukufu viumbe kwaajili yake, dua inaonyesha uwezo wa Mwenyezi Mungu na upana wa elimu yake, na udhaifu wa muombaji na uhitaji wake, kwaajili hii dua ikawa ni katika vitu vitukufu kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.