عن أنس وأبي هريرة رضي الله عنهما مرفوعاً: «لا يُؤْمِنُ أحدُكم حتى أَكُونَ أَحَبَّ إليه مِن وَلَدِه، ووالِدِه، والناس أجمعين».
[صحيح] - [حديث أنس -رضي الله عنه-: متفق عليه.
حديث أبي هريرة -رضي الله عنه-: رواه البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Anasi na Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Hadithi Marfu'u: "Hawezi kuamini mmoja wenu mpaka niwe napendeka kwake zaidi kuliko mtoto wake, na mzazi wake, na watu wote".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Anatueleza Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika hadithi hii: Yakuwa haikamiliki imani ya muislamu, na wala haifikii imani ambayo ataingia nayo peponi bila adhabu, mpaka atangulize mapenzi ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- juu ya mapenzi ya mwanaye na mzazi wake na watu wote, Na hilo ni kwasababu mapenzi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu yanamaanisha: Kumpenda Mwenyezi Mungu; kwasababu Mtume ndiye mfikishaji kutoka kwake, na muongozaji katika dini yake, na mapenzi ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake hayawi sawa ispokuwa kwa kutekeleza maamrisho ya sheria na kuyaepuka makatazo yake, na wala si kwa kuimba kaswida, na kufanya sherehe, na kuremba nyimbo.