+ -

عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رضي الله عنهما:
أَنَّ نَبِيَّ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ كَانَ يَقُولُ عِنْدَ الْكَرْبِ: «لَا إِلَهَ إِلَّا اللهُ الْعَظِيمُ الْحَلِيمُ، لَا إِلَهَ إِلَّا اللهُ رَبُّ الْعَرْشِ الْعَظِيمِ، لَا إِلَهَ إِلَّا اللهُ رَبُّ السَّمَاوَاتِ وَرَبُّ الْأَرْضِ وَرَبُّ الْعَرْشِ الْكَرِيمِ».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 2730]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Bin Abbas -radhi za Allah ziwe juu yao yeye na baba yake-:
Yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa akisema wakati wa matatizo: "Laa ilaaha illa llaahul a'dhwiimul haliim, Laa ilaaha illa llaahu Rabbul A'rshil A'dhwiim, Laa ilaaha illa llaahu Rabbu ssamaawaati warabbul A'rshil kariim" Tafsiri: Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mpole, Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu Mola wa A'rshi tukufu, Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu Mola wa mbingu, na Mola wa ardhi, na Mola wa A'rshi takatifu".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح مسلم - 2730]

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akisema wakati wa kuzidi kwa matatizo na huzuni kwake: "Hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu" Hakuna wa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, "Mtukufu" wa cheo, Mtukufu wa shani, katika dhati yake na sifa zake na majina yake, "Mpole" asiyemharakisha mwenye kuasi kwa kumpa adhabu bali anaichelewesha, na anaweza kumsamehe pamoja nakuwa anauwezo wa kumuadhibu, yeye ndiye muweza Mtukufu juu ya kila kitu ni muweza. "Hapana mola isipokuwa Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa Arshi tukufu" Muumba wa Arshi tukufu, "Hapana mola isipokuwa Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa mbingu na ardhi" na muumba wa mbingu na ardhi, na muumba wa kila kitu ndani yake na mmiliki wake na mrekebishaji wake, na mwenye maamuzi ndani yake kwa namna yoyote aitakayo, "Mola wa Arshi karim" Muumba wa Arshi karim.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kitagalogi Kikurdi Kireno Kiassam
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Uwajibu wa kukimbilia kwa Mwenyezi Mungu kwa dua wakati wa kufikwa na misiba na matatizo.
  2. Kupendeza kuomba dua hii wakati wa matatizo.
  3. Arshi ya Rahmaan (Mwingi wa rehema) aliyotulizana juu yake Aliyetakasika na kutukuka, ndio kiumbe cha juu zaidi kuliko vyote, na kikubwa zaidi na kitukufu zaidi kuliko vyote, na alitoa wasifu wake Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa ni kubwa na ni tukufu.
  4. Zimetajwa mbingu na ardhi pekee; kwa sababu ni katika viumbe vikubwa zaidi katika vile vinavyoonekana.
  5. Amesema Attwayyibi: Ametanguliza sifa hii kwa kumtaja Mola Mlezi ili iendane na kutatua shida; kwa sababu ndilo neno linaloendana na malezi, na ndani yake kuna tahlil (kauli ya Laa ilaaha illa llaah) iliyokusanya tauhidi ambayo ndiyo asili ya kutakasa utukufu wake, na utukufu ambao unaonyesha utimilifu wa uwezo, na upole ambao unaonyesha kuwa na elimu, kwa sababu mjinga hatuwezi kuvuta picha kuwa anaweza kuwa na upole wala ukarimu kwa vitu asivyovijua, nazo ndio asili ya sifa na ukarimu.