عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعًا: «السَّاعِي على الأَرْمَلَةِ والمِسْكِينِ، كالمُجَاهِدِ في سبيل الله». وأَحْسَبُهُ قال: «وكالقائم الذي لا يَفْتُرُ، وكالصائم الذي لا يُفْطِرُ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu zimfikie- Hadithi Marfu'u: "Mwenye kwenda mbio kuwasaidia wajane na masikini, ni kama mwenye kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu" Na nina dhani alisema: "Ni kama anayesimama usiku asiyechoka, au mfungaji asiyefuturu".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume rehema na Amani zimfikie kuwa yule anayesimamia maslahi ya mwanamke aliyefiwa mumewe, na masikini mwenye uhitaji na akawapa matumizi, yeye katika malipo ni kama mpiganaji katika njia ya Mwenyezi Mungu, na ni kama mwenye kusali usiku asiyechoka kuambatana na ibada, na ni kama mfungaji asiyekula.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Sababu ya kuunganishwa mwenye kuwasimamia wajane na masikini kwa yale yanayowafaa na kuwahifadhi- kuunganishwa kwake na- mpiganaji na msimamaji wa usiku, Nikuwa kudumu katika matendo mema kama haya inahitaji kupambana na nafsi na shetani.
  2. Kuhimizwa juu ya kutatua matatizo ya wanyonge na kuziba mapungufu yao na haja zao, na kulinda heshima zao.
  3. Pupa ya sheria ya Uislamu juu ya umoja wa waislamu na kutoshelezana kwao na kusaidizana kwao mpaka liwe na nguvu jengo la Uislamu.
  4. Ibada inakusanya kila amali njema.
  5. Ibada: Ni jina linalokusanya kila analolipenda Mwenyezi Mungu na kuliridhia katika matendo mema ya wazi na ya siri.