عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعًا: «السَّاعِي على الأَرْمَلَةِ والمِسْكِينِ، كالمُجَاهِدِ في سبيل الله». وأَحْسَبُهُ قال: «وكالقائم الذي لا يَفْتُرُ، وكالصائم الذي لا يُفْطِرُ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu zimfikie- Hadithi Marfu'u: "Mwenye kwenda mbio kuwasaidia wajane na masikini, ni kama mwenye kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu" Na nina dhani alisema: "Ni kama anayesimama usiku asiyechoka, au mfungaji asiyefuturu".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Anaeleza Mtume rehema na Amani zimfikie kuwa yule anayesimamia maslahi ya mwanamke aliyefiwa mumewe, na masikini mwenye uhitaji na akawapa matumizi, yeye katika malipo ni kama mpiganaji katika njia ya Mwenyezi Mungu, na ni kama mwenye kusali usiku asiyechoka kuambatana na ibada, na ni kama mfungaji asiyekula.