عن أبي أمامة صُدي بن عجلان الباهلي رضي الله عنه قال: سَمِعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يَخطُبُ في حَجَّة الوَدَاع، فقال: «اتَّقُوا الله، وصَلُّوا خَمسَكُم، وصُومُوا شَهرَكُم، وأَدُّوا زَكَاة أَموَالِكُم، وأَطِيعُوا أُمَرَاءَكُم تَدخُلُوا جَنَّة رَبِّكُم».
[صحيح] - [رواه الترمذي وأحمد وابن حبان. تنبيه: عند أحمد بدل اتقوا: [اعبدوا ربكم]، وعندهما: (ذا أمركم) أما (أمراءكم) فلفظ ابن حبان]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu umama sudai bin Ajlani Al baahiliy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema nilimsikia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- akihutubu katika hija ya kuaga, akasema: "Mcheni Mwenyezi Mungu na mswali swala zenu tano, na mfunge mwezi wenu, na mtekeleze zaka za mali zenu, na muwatii viongozi wenu, mtaingia pepo ya Mola wenu".
Sahihi - Imepokelewa na Ibnu Hibaan

Ufafanuzi

Katika hija ya kuaga alihutubia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- siku ya Arafa, na akahutubia siku ya kuchinja, na akawapa mawaidha watu na akawakumbusha, na hotuba hii ni katika hotuba zilizoko katika mpangilio ambazo ni sunna kwa muongozaji wa mahujaji awahutubie watu kama alivyowahutubia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-, na ilikuwa miongoni mwa yale yaliyotajwa katika moja ya hotuba zake katika hija ya kuaga ni haya yafuatayo: "Enyi watu mcheni Mola wenu", akaamrisha Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake watu wote wamuogope Mola wao aliyewaumba, na akawakunjulia neema zake, na akawaandaa kwaajili ya kukubali ujumbe wake, akawaamrisha wamche Mwenyezi Mungu Mtukufu. Na aliposema: "Na msali swala zenu tano" Yaani swalini swala tano ambazo kazifaradhisha Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka kwa Mjumbe wake -Rehema na Amani ziwe juu yake-. Na aliposema: "Na fungeni mwezi wenu" Yaani: Mwezi wa ramadhani. Na aliposema: "Na tekelezeni zaka zenu" Yaani: Wapeni wenye kustahiki na wala msizifanyie ubahili. Na aliposema: "Na muwatii viongozi wenu" Yaani wale aliowafanya Mwenyezi Mungu kuwa viongozi kwenu, na hii inakusanya viongozi wa mikoa na miji, na inajumuisha kiongozi mkuu: Yaani kiongozi wa nchi nzima, jambo la msingi kwa raia ni kuwatii pale pasipomuasi Mwenyezi Mungu, Ama katika kumuasi Mwenyezi Mungu haitakiwi kuwatii hata kama wataamrisha hivyo; kwasababu kumtii kiumbe hakutangulizwi juu ya kumtii Muumba -Aliyetakasika na kutukuka- Nakuwa atakayeyafanya mambo haya yaliyotajwa katika hadithi basi thawabu zake au malipo yake ni pepo. Na malipo ya atakayefanya hivyo ni pepo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama