+ -

عَنْ مَعْقِلِ بْنِ يَسَارٍ رضي الله عنه أَنَّ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:
«الْعِبَادَةُ فِي الْهَرْجِ كَهِجْرَةٍ إِلَيَّ».

[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 2948]
المزيــد ...

Kutoka kwa Ma'qal bin Yasari -radhi za Allah ziwe juu yake- hakika Mtume rehema na amani za Allah ziwe juu yake alisema:
"Kufanya ibada katika (nyakati) za vita vurugu na mauaji ni kama kuhama kuja kwangu".

[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 2948]

Ufafanuzi

Ameelekeza Mtume rehema na amani ziwe juu yake katika nyakati za vurugu na fitina na mauaji na kuparaganyika kwa mambo ya watu katika ibada na kushikamana nayo, na kwamba malipo yake ni kama kuhama kwenda kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake, na hii ni kwa sababu watu hughafilika nayo, na hawatengi muda ila mtu mmoja mmoja.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Kiassam
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Himizo la kufanya ibada na kuelekea kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu nyakati za fitina; kwa ajili ya kujilinda na fitina, na kujihifadhi na ufisadi.
  2. Kumebainishwa fadhila za kufanya ibada nyakati za fitina na nyakati za watu kughafilika.
  3. Inapaswa kwa muislamu ajitenge mbali na mazingira ya fitina na kughafilika.